Thursday, October 25, 2012


                      IDADI YA WATUMIAJI WA FACEBOOK TANZANIA

Mpaka kufikia leo tarehe 25 oktoba ya 2012,idadi ya watumiaji wa mtandao wa Facebook Tanzania inafikia watu 672,160. Na Tz ni nchi ya 96 kati ya nchi 213 kuwa na idadi ya watu wengi wanaotumia Facebook.
Nchi ya kwanza ni Marekani na ina jumla ya watumiaji 167,263,320 na nchi ya mwisho ni Vatican ambayo inawatumiaji 20 tu.
Kwa Afrika Misri ndio inaongoza ikiwa na watumiaji zaidi ya milioni 11,ikifuatiwa na Nigeria yenye watumiaji milioni 6. Na nchi ya mwisho Afrika kuwa na watumiaji wachache ni Sao tome & Principle yenye watumiaji wanaofikia 6000 tu.
Hasheem Thabeet ndio celebrity mwenye fansi wengi zaidi Tanzania,ambao ni kiasi cha 39,551. Na brand zenye mashabiki wengi ni Tigo,Midcom,Ndovu na Samsung. Huku maeneo yenye 'likes' nyingi zaidi ni kilimanjaro,Kilimanjaro International Airports,mlimani city,Double tree by Hilton hotel na southern sun hotel.
Asilimia 71 ya watumiaji ni wanaume na asilimia 29 tu ndio wanawake.

No comments:

Post a Comment