Thursday, September 27, 2012

RICK ROSS KUTUA TANZANIA A.K.A BONGO TAREHE 6 OKTOBA

Rapper bilionea kutoka USA William Robert a.k.a Rick Ross anatarajia kupiga show nchini Tanzania tarehe 6 mwezi oktoba. Rapper huyo ambae album yake aliyoachia tarehe 31 july imefanikiwa kushika namba moja katika chati za muziki zenye kuheshimika za Billiboard. Ni miongoni mwa wasanii wa marekani wenye kutajwa kuwa na mafanikio katika upande wa muziki na biashara. Rick Ross anamiliki kampuni ya muziki ya Maybach Music Group ambayo inamkataba na Kampuni ya Warner Bross Music Group ambao Roza aliwahi kueleza wakati fulani kuwa ni mkataba wenye thamani ya dola za marekani milioni 25. Huku akiwa ndio CEO wa MayBach Music Group ambayo inasimamia wasanii maarufu akiwemo Meek Mill,Wale,French Montana,Rockie Fresh na wengine kibao.
Pia Rick Ross ana miliki mgahawa wa Boss Wings ambayo ni sehemu ya migahawa maarufu duniani ya Wing Stop. Wakati huo huo akiwa na mikataba kibao ikiwemo na kampuni ya Reebok,Ciroc vodka na kadhalika.
Katika jarida la forbes mwaka huu alitajwa kama miongoni mwa wasanii 20 waliotengeneza pesa nyingi kuanzia mwaka jana hadi mwaka huu.

No comments:

Post a Comment