Monday, September 3, 2012

                     
                          NINI MAKOSA YAKE HUYU MWANDISHI WA HABARI?
Anakumbana na mauti tena ya kinyama wakati akiwa kazini,je ni lipi kosa lake?
Ukitazama vizuri utaona kuwa Bw. Daudi akiwa amemkumbatia mmoja wa maaskari na inavyoonekana alikuwa anapigwa na askari wengine huku huyo askari aliyemkumbatia akionekana kuwazuia wengine kutoendelea kumshambulia. Na hapo hapo kuna askari mwingine mbele yake akiwa ameshika bunduki.
Hapa kwa mujibu wa mashuhuda na vyombo vingine vya habari,hapa ilikuwa ni kiasi cha dakika zisizozidi 20 wakati akiwa kazini na kamera yake akiendelea kuchukua matukio kadhaa yaliyokuwa yakiendelea.
Sasa je kama ni mlipuko,huo mlipuko ulimpata yeye tu ukawakosa askari wengine? Na kama uliwakosa Askari wengine mbona kuna picha inaonekana alikuwa amemkumbatia askari mwingine na askari huyo akionekana kama anamwokoa na wakati huo huo kuna askari mwingine akiwa ameshika bunduki.
Tazama vizuroi hii picha hapa chini.
Kwa fikra za kawaida tu,sitaki kusimama upande wowote iwe ni serikali,wananchi au Chama cha CHADEMA. Kinachoumiza zaidi ni kuwa huyu mwandishi wa habari alikuwa kazini.
JE HUYU MWANDISHI ALIKUWA ANA MAKOSA GANI?


No comments:

Post a Comment