Wednesday, August 29, 2012


KILICHOTOKEA MOMBASA KISITOKEE TENA MOMBASA WALA PENGINE POPOTE


Sheikh Aboud Rogo alikuwa shujaa na role model kwa wengine lakini pia alikuwa adui kwa wengine. Ninalazimika kusema hivyo,na si kwa ubaya bali kwa wema. tukio la mauaji yake limenisikitisha sana.
Naweza nikasema ni mauaji ya kinyama ambayo usingetegemea!Ni tukio lililotokea tena mbele ya familia yake. Kama ilivyosikika katika vyombo mbalimbali vya habari kuwa Sheikh Aboud Rogo alikuwa anampeleka mkewe hospitali na alikuwa kwenye gari pamoja na baba mkwe wake na mtoto wake.
Nimelazimika kusema Sheikh Aboud Rogo alikuwa adui na shujaa kwa watu wawili tofauti kwa sababu;
Inajulikana wazi alikuwa anachukiwa na Marekani kutokana na kumtuhumu kujihusisha na kundi la Al-shabab la Somalia. Lakini pia nalazimika kusema pia alikuwa ni shujaa kwa watu wengine hususani baadhi ya Waislamu.
Sasa baada ya kifo chake tumeshuhudia makanisa yakichomwa,magari ya serikali pia yakichomwa.
SOTE NI NDUGU TOFAUTI ZETU ZA KIDINI ZISITUSABABISHE TUKACHUKIANA AU TUKAJIONA NI BORA ZAIDI YA WENGINE.
Mombasa ni jiji lililopo karibu na Tanga Tanzania na kinachotokea Mombasa kinatuhusu sisi pia Watanzania sio kwa sababu Mombasa ni jirani zetu bali pia tuna mahusiano ya karibu sana,kibiashara na hata kindugu kwani kuna watu wameolewa na kuoa Mombasa.

                                          Hapo ni enzi za uhai wake

Baada ya kifo chake......Ebu tazama huyo mtoto anavyolia,unafikiri hiyo taswira inaweza kupotea akilini mwake kwa muda mfupi?..........

LET US PRAY FOR THE PEACE OF EAST AFRICA

No comments:

Post a Comment