Sunday, September 16, 2012

         

         BAKHRESSA MMOJA WA MATRILIONEA WAKUBWA AFRICA.


Kwa mujibu wa jarida maarufu duniani,Said Salim Bakhressa ni miongoni mwa matajiri wakubwa Africa ambao utajiri wao unaongezeka kwa kasi. Kwa mujibu Forbes Magazine Kampuni yakeya Bakhressa Group inatengeneza mauzo yanayohfikia dola za marekani milioni 800 sawa na shilingi za Tanzania trilioni 1.2.
Kama ukipata nafasi ya kujua au kusimuliwa namna mzee huyu alivyoanza inaweza ikakushangaza lakini pia ikakupa nguvu. Kwani wahenga wanasema ''polepole ndio mwendo''. Mzee alianza na kuuza viazi na baadae alifungua migahawa. 
Hii ni changamoto na inspiration kwa vijana wenzangu. Ninachoamini ni kuwa ukifanya kile unacokipenda na ukakifanya kwa moyo wote  na bidii yote utafanikiwa.
Nakumbuka Mama yangu aliponiambia kuwa wakati nikiwa mtoto mdogo kwenye miaka ya themanini mwishoni na tisini mwanzoni alipokuwa ananipeleka hospitali ya Muhimbili tulikuwa tunakula kwenye migahawa yake. Na sasa nimekuwa mkubwa kabisa bado ninakunywa na kutumia bidhaa ambazo amebuni. 

No comments:

Post a Comment