tag:blogger.com,1999:blog-37300421895257418662024-03-05T10:26:31.671+03:00POPOTE TZTEKNOLOJIA,BURUDANI NA AFYA!!NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.comBlogger82125tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-44522692349193125362012-10-25T11:43:00.000+03:002012-10-25T12:24:21.845+03:00<div style="color: red;">
<br /></div>
<div style="color: red;">
<span style="font-size: large;">IDADI YA WATUMIAJI WA FACEBOOK TANZANIA</span></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhLNLF2l6A0uNxmF0VA-nlUZfieci-7AU45rJhnyIoTLlz0gugTscvhAuub-agCa0wErtYh5qdOljiQ962zVohtk3iniiH7-lsc90qgp2koVnAOXYDUPAcTKsnViS4AQjk4mq_mgNOLrgJt/s1600/Facebook-logo1.jpeg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="213" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhLNLF2l6A0uNxmF0VA-nlUZfieci-7AU45rJhnyIoTLlz0gugTscvhAuub-agCa0wErtYh5qdOljiQ962zVohtk3iniiH7-lsc90qgp2koVnAOXYDUPAcTKsnViS4AQjk4mq_mgNOLrgJt/s320/Facebook-logo1.jpeg" width="320" /></a></div>
<br />
Mpaka kufikia leo tarehe 25 oktoba ya 2012,idadi ya watumiaji wa mtandao wa Facebook Tanzania inafikia watu 672,160. Na Tz ni nchi ya 96 kati ya nchi 213 kuwa na idadi ya watu wengi wanaotumia Facebook.<br />
Nchi ya kwanza ni Marekani na ina jumla ya watumiaji 167,263,320 na nchi ya mwisho ni Vatican ambayo inawatumiaji 20 tu.<br />
Kwa Afrika Misri ndio inaongoza ikiwa na watumiaji zaidi ya milioni 11,ikifuatiwa na Nigeria yenye watumiaji milioni 6. Na nchi ya mwisho Afrika kuwa na watumiaji wachache ni Sao tome & Principle yenye watumiaji wanaofikia 6000 tu.<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
</div>
Hasheem Thabeet ndio celebrity mwenye fansi wengi zaidi Tanzania,ambao ni kiasi cha 39,551. Na brand zenye mashabiki wengi ni Tigo,Midcom,Ndovu na Samsung. Huku maeneo yenye 'likes' nyingi zaidi ni kilimanjaro,Kilimanjaro International Airports,mlimani city,Double tree by Hilton hotel na southern sun hotel.<br />
Asilimia 71 ya watumiaji ni wanaume na asilimia 29 tu ndio wanawake. <br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-28846650130334140432012-10-09T20:46:00.001+03:002012-10-09T20:46:30.896+03:00TAARIFA YA UCHUNGUZI WA KIFO CHA MWANDISHI WA HABARI WA CHANNEL TEN BW. DAUD MWANGOSI<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi0gPKD45ss3Wwfy9VJfFhe8_iTu0uCbMg28zr3_4LdlF_5PTbFiOBCvJLaGB_Kz2M4Tj6KMxUzrrQYExM6XaWvtfXIfPh-p3UmUnAOH9FuXxwhjAKSZEvZvE3EXogOrligzvHiGyKxUYRf/s1600/849116793.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi0gPKD45ss3Wwfy9VJfFhe8_iTu0uCbMg28zr3_4LdlF_5PTbFiOBCvJLaGB_Kz2M4Tj6KMxUzrrQYExM6XaWvtfXIfPh-p3UmUnAOH9FuXxwhjAKSZEvZvE3EXogOrligzvHiGyKxUYRf/s320/849116793.jpg" width="318" /></a></div>
<br />
<br />
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>TAARIFA YA UCHUNGUZI WA KIFO CHA MWANDISHI WA HABARI WA </strong></span><strong style="color: black;">CHANNEL TEN BW. DAUD MWANGOSI</strong></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>1.0 UTANGULIZI</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Mnamo tarehe 03 Septemba mwaka 2012, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. </strong></span><strong style="color: black;">Dkt. Emmanuel Nchimbi (MB) aliteua Kamati ya watu watano kufanya uchunguzi </strong><strong style="color: black;">kuhusiana na kifo cha mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel </strong><strong style="color: black;">Ten, marehemu Daud Mwangosi, kilichotokea tarehe 02 Septemba 2012, katika Kijiji </strong><strong style="color: black;">cha Nyololo,Wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa. Kituo cha kazi cha marehemu Daud </strong><strong style="color: black;">Mwangosi kilikuwa mkoa wa Iringa ambapo pia alikuwa Mwenyekiti wa Klabu ya </strong><strong style="color: black;">Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Iringa (IPC).</strong></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Wajumbe wa Kamati hiyo ni:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Jaji (Mst.) Steven Ihema – Mwenyekiti</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Bibi Pili Mtambalike – Mjumbe</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kanali (Dkt. Eng) Wema Wilson Wekwe – Mjumbe</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Bwana Theophil Makunga – Mjumbe</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Naibu Kamishna wa Polisi Issaya Juma. Mngulu – Katibu</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Sekretarieti ya Kamati ni:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Bi. Edith T. Assenga – Wizara ya Mambo ya Ndani</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Bwana Nasoro H. Msumi – Wizara ya Mambo ya Ndani</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>2.0 HADIDU ZA REJEA</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kamati ilipewa Hadidu za rejea zifuatazo:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-
Uhalali wa mkusanyiko ulioitishwa na CHADEMA eneo la Nyololo,Wilaya ya
Mufindi, Mkoa wa Iringa tarehe 02 Septemba, 2012 na kuwepo kwa uvunjifu
wa amani.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Kama yalikuwepo makubaliano au maelekezo kuhusu mikutano ya hadhara au maandamano nchini katika kipindi cha Sensa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Mazingira
yaliyosababisha Jeshi la Polisi kutumia nguvu iliyosababisha kifo cha
Marehemu Daud Mwangosi na wengine kuumizwa, na uwiano wa nguvu hiyo na
tukio.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Madai
ya kuwepo uhasama kati ya Jeshi la Polisi na Waandishi wa Habari Mkoa
wa Iringa na chanzo cha uhasama huo. Aidha kuna madai ya kuwepo kwa
orodha ya waandishi watatu (3) ambao Jeshi la Polisi limepanga
kuwashughulikia.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Uwepo
wa Sheria, Kanuni au Taratibu zinazotoa uwezo kwa Jeshi la Polisi
kuzuia mikusanyiko inayoitishwa na Vyama vya Siasa na Mamlaka ya Rufaa
endapo vyama hivyo havitaridhika na amri hizo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Hali ya Mahusiano kati ya Jeshi la Polisi na Vyama vya Siasa nchini katika Utendaji kazi wao na Utii wa Sheria.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>3.0 MUDA WA UCHUNGUZI</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kamati
ilipewa muda wa siku 19 kuanzia tarehe 11 Septemba 2012 iwe
imekamilisha uchunguzi na kuwasilisha Ripoti yake ifikapo tarehe 02
Oktoba 2012.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<br /></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>4.0 NJIA ZILIZOTUMIKA KUFANYA UCHUNGUZI:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>4.1 Mahojiano na watu mbalimbali waliokuwepo kwenye tukio.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>4.2 Kupitia nyaraka na vielelezo mbalimbali.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>4.3 Kutembelea eneo la tukio.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>4.4
Majadiliano na vikundi mbalimbali (viongozi wa dini ngazi ya kijiji na
wilaya hadi ya mkoa; viongozi wa vyama vya siasa kwenye ngazi ya kijiji,
wilaya, mkoa na Taifa, viongozi wa serikali ngazi ya kijiji, wilaya,
mkoa, Taifa) na wanakijiji wa Nyololo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>5.0 UCHUNGUZI</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kamati
ya Uchunguzi ilifanya mahojiano na watu mbalimbali ikiwa pamoja na
watendaji wa serikali hususan Kamati za Ulinzi na Usalama ngazi ya
wilaya Mufindi na mkoa wa Iringa viongozi wa Jeshi la Polisi viongozi wa
vyama vya Siasa, Viongozi wa Madhehebu ya Dini, Waandishi wa Habari na
wananchi wa kawaida (ngazi ya Kijiji, Kata, Wilaya, Mkoa na Taifa).</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>6.0. YALIYOJITOKEZA</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Baada
ya Kamati kukutana na makundi ya watu mbalimbali katika Mkoa wa Iringa
na Viongozi wa Vyama vya Siasa wa kitaifa jijini Dar es Salaam, mambo
kadhaa yalijitokeza na baadhi yao ni:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Hofu
ya kutoweka kwa amani miongoni mwa viongozi na wananchi hasa katika
mikutano na maandamano ya siasa ambayo yameanza kuota mizizi ya uvunjifu
wa amani na mengine kusababisha mauaji. Viongozi na wananchi wengi
waliotoa maoni yao mbele ya Kamati wameonyesha hofu kuwa hali hiyo
isipodhibitiwa mapema inaweza kulipeleka pabaya Taifa letu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kuna walakini wa mahusiano kati ya waandishi wa habari na Jeshi la Polisi mkoani Iringa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Uwepo
wa utashi wa makusudi/dhati kwa viongozi wa vyama vyote vya siasa
kuweka mbele maslahi ya taifa badala ya maslahi ya vyama.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Umuhimu
wa Ushirikiano na mahusiano baina ya vyombo vya serikali, vyama vya
siasa, wanahabari na wananchi kwa ujumla badala kuonyeshana ubabe ambao
umetufikisha hapo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Haja ya kufanya mabadiliko ya kisheria katika mfumo wa usimamizi na utendaji wa masuala ya siasa nchini</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-
Haja ya kuwa na mabadiliko ya kimfumo katika Jeshi la Polisi badala ya
ulioko sasa ambao kwa maoni ya baadhi ya watu waliozungumza na Kamati ni
wa kitaifa zaidi na kuacha serikali za mitaa bila ya wajibu wa kulinda
usalama wa raia na mali zao.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kwamba nguvu kubwa inatumika na vyombo vya dola/usalama dhidi ya raia na hivyo kupunguza imani ya jamii kwa vyombo hivyo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kupungua kwa maadili/uzalendo miongoni mwa Watanzania kuanzia viongozi hadi wananchi hususan kwenye shughuli za kisiasa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Haja
ya kusisitiza elimu ya uraia kwa jamii kuanzia kwa watoto hadi kwa watu
wazima hasa wakati huu wa mfumo wa vyama vingi ili kujenga umoja wa
kitaifa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kuwepo kwa mikutano na maandamano ya vyama vya siasa yasiyokuwa na kikomo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Muonekano wa Jeshi la Polisi mbele ya jamii.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>7.0. MATOKEO YA UCHUNGUZI KUTOKANA NA HADIDU ZA REJEA</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>7.1
Kuhusu “Uhalali wa mkusanyiko ulioitishwa na CHADEMA eneo la Nyololo,
Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa tarehe 02 Septemba 2012 na kuwepo
uvunjifu wa amani”, uchunguzi wa Kamati umebaini yafuatayo:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Tarehe
30 Agosti 2012 CHADEMA iliandika barua, Ofisi ya Mkuu wa Polisi Wilaya
ya Mufindi kutoa taarifa kuhusu ratiba ya mikutano ishirini na sita (26)
kwenye majimbo ya Mufindi Kusini na Kaskazini tarehe 02-03 Septemba
2012. Awali ratiba ya mikutano hiyo ilikubaliwa, lakini baadaye siku
hiyo ya tarehe 01 Septemba 2012 mikutano hiyo ilisitishwa kwa barua
Kumb. Na MFG/A.24/9/54 kutokana na kuongezwa siku za zoezi la Sensa ya
watu na Makazi hadi tarehe 08 Septemba 2012.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>CHADEMA
walikataa kusitisha ratiba ya mikutano hiyo kama inavyothibitishwa na
Justin Leornard Mpotwa Katibu wa Wilaya ya Mufindi kwa barua yake Kumb.
Na CDM/M4/002/Vol.01/2012 ya tarehe 01 Septemba 2012 kuwa “pia tunaomba
ieleweke bayana kwamba kisheria shughuli zetu hazina mwingiliano na wala
kuhusiana na program iliyoongezwa ya Sensa. Kwa barua hii tunakuarifu
kuwa mikutano tuliyokutaarifu kuifanya kuanzia kesho tarehe 02 septemba
2012 itaendelea kama ilivyopangwa – CHADEMA VEMA”.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Aidha
kuwepo kwa zuio la mikutano ya Siasa ya CHADEMA Mkoani Iringa wakati wa
zoezi la Sensa ya Watu na Makazi linathibitishwa na Amri ya Utendaji
(Operation Order) ya Kamanda wa Polisi Mkoa (SACP Michael Kamuhanda) ya
tarehe 01 Septemba 2012. Amri ya Utendaji ambayo ni amri halali
ilitolewa ili “kuzuia shughuli za Siasa (mikutano na maandamano) kipindi
cha zoezi la kitaifa la Sensa kuanzia tarehe 25 Agosti 2012 hadi 08
Septemba 2012”. Uhalali wa Amri/Zuio hili ulithibitishwa pia na Msajili
wa Vyama vya Siasa nchini katika barua yake Kumb Na. DA. 112/ 123/ 01/
34 ya tarehe 28/08/2010 na wakati wa mahojiano na Kamati ya uchunguzi
tarehe 22 Septemba 2012.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Licha
ya zuio/amri hii Viongozi wa CHADEMA walikataa kutii amri hiyo.
Kutokana na taarifa hizi, Kamati ya Uchunguzi inathibitisha kwamba
hapakuwepo na uhalali wa mkusanyiko/mkutano ulioitishwa na CHADEMA eneo
la Nyololo, Wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa tarehe 02 Septemba 2012.
Kuhusu kuwepo kwa uvunjifu wa amani Kijijini Nyololo tarehe 02 Septemba
2012 Kamati ya Uchunguzi ilibaini mambo yafuatayo:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Tukio
la kuuawa kwa Daud Mwangosi jioni ya tarehe 02 Septemba 2012 lilitokea
baada ya Operesheni ya Jeshi la Polisi kumalizika. Hii ni kwa mujibu wa
maelezo ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza
Ghasia Mkoa wa Iringa na Joseph Senga Mpiga picha/Mwandishi Tanzania
Daima.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-
Kitendo cha kutotii amri halali ya Kamanda wa Polisi kuagiza wafuasi wa
CHADEMA watawanyike kutoka kwenye eneo la ofisi ya Kata ya CHADEMA
ilikuwa chanzo cha vurugu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Uamuzi
wa CHADEMA kung’ang’ana kukusanyika isivyo halali eneo la Nyololo
ikizingatiwa kuwepo kwa ujumbe wa SMS kutoka kwa Dkt. Slaa, Katibu wa
CHADEMA uliosema, “IGP nasubiri simu yako. Wajulishe Polisi wako waandae
risasi za kutosha, mabomu ya kutosha. Mtakuwa na karamu ya mauaji na
kisha kusherehekea, mjiandae kwa kwenda mahakama ya Den Hague. Ni
afadhali tufe kuliko manyanyaso haya”. Dr. Slaa. : ujumbe huu ukiashiria
umwagaji wa damu ni ushaidi tosha kuwepo kwa uvunjifu wa amani. CHADEMA
ndiyo Chanzo cha vurugu na uvunjifu wa amani Kijijini Nyololo tarehe 02
Septemba 2012.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>7.2
Kama yalikuwepo makubaliano kuhusu mikutano ya hadhara au maandamano
nchini katika kipindi cha Sensa. Katika kuzungumzia hoja hii tukianzia
na Uongozi wa Serikali na Vyama vya Siasa ngazi ya Wilaya, Mkoa hadi
Taifa, Kamati ya Uchunguzi ilithibitisha kuwepo kwa maagizo ya
kusimamisha mikutano/maandamano ya Vyama vya Siasa wakati wa kipindi cha
Sensa ya Watu na Makazi yaliyotolewa na Msajili wa Vyama vya Siasa
nchini, na kuongezwa muda wa Sensa hadi tarehe 08 Septemba 2012 na
Kamishna wa Sensa hapo tarehe 01 Septemba 2012.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Aidha
hoja hii imethibitika kwamba Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kwa
barua yake yenye Kumb Na DA. 112/ 01/ 34 ya terehe 28 Agosti 2012 kwenda
kwa Makatibu Wakuu wa Vyama vya Siasa akiwasihi kusimamisha shughuli
zote za mikutano na maandamano ya Vyama vyao kwa kipindi chote cha Sensa
ya Watu na Makazi. Aidha kwa mujibu wa Gazeti la Serikali Na 29 VOL 93
ya tarehe 20 Julai 2012, Mhe. Rais, JAKAYA MRISHO KIKWETE kwa mamlaka
aliyopewa chini ya kifungu namba 14 cha Sheria ya Takwimu sura 351
alielekeza kwamba Sensa ya Watu na Makazi itafanyika kuanzia tarehe 26
mwezi wa nane, mpaka tarehe 08 mwezi wa tisa mwaka 2012.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kamishna
wa Sensa aliratibu zoezi la Sensa ya Watu na Makazi kumalizika ifikapo
tarehe 01 Septemba 2012. Hata hivyo kutokana na tathmini aliyofanya,
kazi hiyo ilikuwa imekamilika kwa asilimia 95%. Hivyo tarehe 01 Septemba
2012 alitoa taarifa kwa Vyombo vya Habari kwamba ili kila mwananchi
apate nafasi ya kuhesabiwa watu watakaokuwa wamesalia ambao ni chini ya
5% wanaombwa kutoa ushirikiano ili zoezi hili likamilike. Hivyo, wale
wote mmoja mmoja waliobakia wataendelea kuandikishwa hadi tarehe 08
Septemba 2012.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa
upande wake Inspekta Jenerali wa Polisi kwa ujumbe wa simu Kumb Na
S8.7/ 2/ A/ VOL XIV/ 59 ya tarehe 28/08/2012, pia simu yake Kumb Na
C.28/ B/ 44 ya terehe 01/ 09/ 2012 aliwaelekeza Makamanda wa Polisi wa
Mikoa kutoruhusu mikutano na maandamano wakati huu wa zoezi la Sensa ya
Watu na Makazi mpaka litakapokamilika tarehe 08 Septemba 2012.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kimsingi
Kamati ya uchunguzi imethibitisha kwamba maelekezo kwa Vyama vya Siasa
kutoendesha shughuli za mikutano ya hadhara au maandamano yalitolewa kwa
mujibu wa Sheria.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>7.3
Mazingira yaliyosababisha Jeshi la Polisi kutumia nguvu iliyosababisha,
kifo cha marehemu Daud Mwangosi na wengine kuumizwa, na uwiano wa nguvu
hiyo na tukio.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Hoja
kuwa Polisi walitumia nguvu kubwa katika kudhibiti mkutano wa CHADEMA
iliungwa mkono na Viongozi wa Serikali ya Kijiji, Viongozi wa dini na
Viongozi wa siasa Kijijini Wilayani na Mkoani pamoja na Waandishi wa
Habari. Hata hivyo Kamati za Ulinzi na Usalama Wilaya na Mkoa na
Viongozi wa Jeshi la Polisi waliona nguvu hizo ni za mazingira ya hali
ilivyokuwa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Uchunguzi
wa suala hili umebaini kwamba tarehe 02 Septemba 2012 muda wa saa 10 za
jioni huko eneo la Sokoni, Kijiji cha Nyololo kulikuwepo na mkutano
usio halali ulioandaliwa na viongozi wa CHADEMA. Upo ukweli kwamba
uongozi wa Polisi ulitoa ilani kuamuru wafuasi wa CHADEMA waliokuwepo
mkutanoni hapo waondoke la sivyo nguvu itatumika. Walikaidi amri hiyo na
ilipoagizwa viongozi wakamatwe ndipo walianza kurusha mawe kwa Askari
Polisi. Baadhi ya Askari walijeruhiwa, akiwamo G 9934 PC Mgaka alivunjwa
mkono wa kulia. Pia kofia (helmet) tatu ziliharibiwa. </strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kutokana
na hali hiyo amri ya kupiga mabomu ya machozi na ya kishindo ilitolewa,
kwa mujibu wa Kifungu 77 hadi 79 cha Kanuni za Adhabu, Sura ya 16 – R.E
2002. Operesheni hii ilimalizika baada ya kukamatwa viongozi na wafuasi
wa CHADEMA jumla yao saba.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Baada
ya zoezi hilo kukamilika Askari Polisi walioshiriki kwenye Operesheni
waliamriwa kuingia katika magari tayari kwa kuondoka. Wakati Askari
wakipanda kwenye magari kishindo kikubwa kilitokea umbali wa zaidi ya
mita 100 kutoka sehemu ambayo operesheni ilikuwa inafanyika na
iligundulika kwamba kishindo kile kimesababisha kifo cha Mwandishi wa
Habari Daud Mwangosi.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Upelelezi
wa awali pamoja na picha za mnato unaonyesha kwamba marehemu alikuwa
amemkumbatia Mkuu wa Polisi Kituo cha Mafinga ASP Assel Mwampamba na
huku akiwa amezungukwa na Askari Polisi wasiopungua sita ambao licha ya
kumzunguka marehemu Daud Mwangosi kuna madai yaliyotolewa na mwandishi
wa Habari Joseph Senga kwamba, Askari Polisi hao walikuwa wanamshambulia
marehemu kwa kumpiga, ndipo askari mmoja aliyetambuliwa kuwa ni G 2573
PC Pasificus Cleophace Simon alifyatua Bomu la kishindo na kusababisha
kifo cha Daud Mwangosi.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Tukio
hili linaweza kugawanyika katika sehemu mbili: sehemu ya kwanza ni
wileamapamebas(mni ya kutawanya watu na ya pili ni ile ya mauaji ya Daud
Picha Namba 15: Askari Polisi wakimpiga Marehemu Daud Mwangosi, huku
OCS M wenye kifimbo) akijaribu kuwazuia. Mwangosi. Katika tukio la
kwanza idadi ya Askari walioshiriki ni Sekisheni Tukio hili linaweza
kugawanyika katika sehemu mbili: sehemu ya kwanza ni lile ya Operesheni
ya kutawanya watu na ya pili ni ile ya mauaji ya Daud Mwangosi.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong> Katika
tukio la kwanza idadi ya Askari walioshiriki ni Sekisheni tatu ambapo
ni askari wasiozidi thelathini. Kwa maelezo yaliyotolewa na Mwandishi wa
Habari mbele ya Kamati, Bw Joseph Senga anaeleza kuwa watu
walishatawanyika na hali kutulia mara baada ya Operesheni hii kukamilika
na Polisi kujiandaa kuondoka kwenye eneo la tukio. Tukio la mauaji ya
Daud Mwangosi lilisababishwa na kupigwa bomu la kishindo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Maswali
ya kujiuliza katika tukio la mauaji ni Je, kulikuwepo na uwiano
unaolingana na tukio hili?, Je Palikuwa na uhalali wa kutumia Bomu la
kishindo?, na Je, utumiaji wa Bomu hilo ulikuwa na umuhimu?</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kulingana na tukio lenyewe majibu ya maswali hayo ni kama ifuatavyo:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Hapakuwa
na uwiano wa Bomu na tukio la mauaji, kwa vile utaratibu wa matumizi ya
bomu hilo unaelekeza kulenga juu usawa wa nyuzi 45 na umbali mita 80
mpaka mita 100.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Hapakuwa na uhalali wa kutumia Bomu la Kishindo kwani lengo la ulipuaji wake ni ili watu waogope na kukimbia.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-
Hapakuwepo umuhimu wa kutumia Bomu la Kishindo kwa sababu hata ingekuwa
ukamataji tayari Askari Polisi wapatao sita walikuwepo eneo la tukio.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa
misingi hiyo Kamati imeona kwamba nguvu iliyotumika mwanzo hadi
kumaliza Operesheni haikuwa kubwa. Kuhusu tukio la kuuawa Bw. Daud
Mwangosi na kuumizwa baadhi ya Askari Polisi halikustahili kabisa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>7.4
Madai ya kuwepo uhasama kati ya Jeshi la Polisi na Waandishi wa Mkoa wa
Iringa na chanzo cha uhasama huo. Aidha madai ya kuwepo kwa orodha ya
waandishi watatu (3) ambao Jeshi la Polisi limepanga kuwashughulikia.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Katika
kupata ukweli wa jambo hili, Kamati ilikutana na wanachama wa Klabu ya
Waandishi wa Habari Iringa na pia iliwahoji Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa
Iringa, Michael Kamuhanda, Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa, Nyigesa Ramadhani
Wankyo na Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia mkoani Iringa Said
Abdallah Mnunka.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Pia,
wakati Kamati inakutana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, ilileta
suala la mahusiano kati ya Polisi na waandishi wa habari na watendaji
wakuu wa serikali wa mkoa wa Iringa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Katika
mkutano na waandishi wa habari, ilionekana kuwa katika thathmini yao
uhusiano kati yao na Polisi hapo mkoani ni mbaya sana. Walieleza matukio
kadhaa ya kunyanyaswa waandishi wa habari wakati wapo kazini, ikiwamo
kupigwa, kutishiwa kuharibiwa na kuharibiwa vifaa vyao vya kazi na hata
kutishiwa maisha ili wasiripoti mambo ambayo Polisi wana maslahi nayo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa
mfano, mwandishi wa habari wa Star TV, Oliver Moto alieleza Kamati
kuwa: “Waandishi wa habari hawana mahusiano mazuri na Jeshi la Polisi,
na hata wanapofika ofisi za Polisi huwa hawapewi ushirikiano. Kutokana
na uhusiano mbaya wanahabari walifanya maandamano tarehe 06 Machi 2012
kupinga unyanyasaji wanaofanyiwa na Jeshi la Polisi hapa Iringa”.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Mwandishi
mwingine wa habari Zulfa Shomari ambaye anaandikia gazeti la Mwananchi
alieleza kuwa kuna matukio kadhaa ambayo Polisi wamewazuia waandishi
kufanya kazi zao mojawapo ni lile ambalo Polisi walikataza kupigwa picha
tukio la kukamatwa kwa pembe za ndovu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kamati
pia iielezwa na mwandishi wa habari wa ITV, Bw. Laurian Mkumbata mkasa
wa kuvunjwa kamera yake na OCD Iringa kwenye tukio moja. Ilibidi OCD
alipe kamera hiyo kwa maagizo ya RPC.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Pia
walisema kuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa hivi sasa ana mawasiliano duni
sana na waandishi wa habari na juhudi za wengi wao kumfuata ili
athibitishe tukio zimekuwa zikishindwa kwani ameweka maagizo getini kuwa
mtu yeyote ambae anataka kumuona ni lazima aeleze anataka kumuona kwa
sababu gani ndipo aruhusiwe kuingia. Kwa sababu hii waandishi wa habari
wengi wamekata mguu kwenda ofisini kwake.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Mwandishi
mmoja wa Ebony FM Bw. Raymond Francis, aliiambia Kamati kuwa yeye
binafsi alitishiwa kuuawa na baada ya kuandaa kipindi kuhusiana na watu
wanaoshukiwa kufanya biashara haramu ya madawa ya kulevya ambao
wanahusiana na baadhi ya Polisi wasio waadilifu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong> Mwandishi
wa Habari Greyson Mgoi wa gazeti la Kwanza Jamii aliiambia Kamati kuna
tukio la kuanguka kwa lori la mafuta eneo la Ifunda karibu na Mafinga
ambapo waliwakuta wananchi na polisi wakichota mafuta kutoka kwenye hilo
gari.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Alisema
kuwa waliamua kupiga picha tukio hilo lakini Polisi waliwakamata na
kuwalazimisha wafute hizo picha walizopiga. Kwa kuogopa shari walikubali
kuzifuta na wakaruhusiwa kuendelea na safari yao.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Waandishi
wa Habari hata hivyo walibainisha kuwa uhusiano wao na Polisi hapo
mkoani ulikuwa mzuri sana kipindi cha uongozi wa RPC Advocate Nyombi.
Walisema kuwa wakati wa RPC Nyombi, alikuwa na utaratibu wa kukutana na
waandishi wa habari na pia alikuwa anafikiwa na waandishi wa habari kwa
urahisi kwa simu au ofisini kwake. Walisema lakini ulianza kuharibika
alipohama na nafasi yake kuchukuliwa na RPC Mangara na kuwa mbaya zaidi
alipokuja Kamuhanda. Walidai kuwa Polisi wa Iringa si waadilifu na
wamekuwa wakijiona kama miungu watu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Waandishi
walieleza Kamati, kitu kilichowaudhi sana ni yale majibu yaliyotolewa
na RPC baada ya mauaji ya Daud Mwangosi ambayo yalionekana yalikuwa ni
ya kupanga ili ukweli usijulikane. Walisema kama si picha zilizotolewa
na waandishi wa habari waliokuwepo kwenye tukio, hawadhani kama umma wa
Watanzania wangepata ukweli wa tukio hilo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Walisema
tarehe 06 Machi 2012, walifanya maandamano ili kupinga manyanyaso ya
Polisi wa mkoani Iringa yaliyopokelewa na Mkuu wa Mkoa. Waandishi wa
Habari mkoani Iringa pia walionyesha masikitiko yao kuwa tangu kutokee
kwa mauji ya Daud Mwangosi, hawajapokea pole kutoka kwa Mkuu wa Mkoa na
watendaji wake wa juu hata kama ni ya “kinafiki”.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa
upande wa pili, yaani Jeshi la Polisi, Kamati ilipata taswira tofauti.
RPC Kamuhanda alisema kuwa yeye anaona mahusiano ya Polisi na waandishi
wa habari kwa ujumla ni mzuri na yeye binafsi amekuwa akikutana na
waandishi wa habari takriban kila siku asubuhi saa nne kuwapa habari.
Pia aliiambia Kamati kuwa waandishi wa habari walishiriki kikamilifu
katika kuripoti michuano ya mpira ya Kikombe cha Kamuhanda yaliyofanyika
mjini Iringa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Msimamo
huo pia ulichukuliwa na viongozi wa juu wa kiutawala akiwemo Mkuu wa
Mkoa Dkt. Christine Ishengoma, Katibu Tawala wa Mkoa Bibi Getrude Mpaka
ambao walisema kuwa hapakuwa na uhasama wowote kati ya Ofisi ya Mkuu wa
Mkoa na Waandishi wa Habari. Wote wawili walisema kuwa walimfahamu
marehemu Daud Mwangosi na aliteuliwa katika kamati kadhaa za kimkoa
ikiwa ni pamoja na ile ya kuandaa Sensa ya Watu na Makazi Mkoani, Kamati
ya Masuala ya Katiba ya Mkoa na Kamati ya Kukuza Utalii ya Mkoa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kuhusiana
na hisia kuwa Mkuu wa Mkoa na watendaji wake hawakujumuika na waandishi
katika msiba wa Daud Mwangosi, Dkt. Ishengoma alisema si kweli
hawajatoa rambirambi zao kwa kifo cha Mwangosi lakini alitoa pole kwa
waandishi wakati ameenda na IGP Mwema kijijini Nyololo na pia kupitia
radio katika kipindi kilichotayarishwa na mwandishi wa habari Francis
Godwin.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Baada
ya kuongea na pande hizo mbili, Kamati imebaini kwamba kuna walakini wa
mahusiano kati ya waandishi wa habari na baadhi ya askari polisi mkoani
Iringa. Kuhusu madai ya kuwepo kwa orodha ya waandishi watatu (3) ambao
jeshi la polisi limepanga kuwashughulikia.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwenye
tukio la Nyololo ambapo mwandishi wa habari Daud Mwangosi aliuawa,
mwandishi wa habari mwengine Godfrey Mushi alipigwa na Polisi na
inasemekana kujeruhiwa vibaya na baadaye kukamatwa na Polisi.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa
mujibu wa Joseph Senga mpiga picha/mwandishi wa habari wa gazeti la
Tanzania Daima ambaye alikuwepo kwenye tukio na kupiga picha, alimuona
marehemu akipita nyuma ya gari moja la Polisi ambalo lilikuwa na baadhi
ya wanachama wa CHADEMA. Punde tu alimwona mtu amezungurukwa na askari
akipigwa lakini hakujua ni nani na yeye aliendelea kupiga picha tukio
hilo mpaka nae alipokamatwa na Polisi watatu ambao walimwuliza kama nae
anataka aende kuungana na mtu anayepigwa pale.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Senga
alisema wakati kipigo kinaendelea, kuna askari mmoja mwenye nyota tatu
(OCS Mwampamba) aliteremka kutoka kwenye gari na kwenda pale ambapo Yule
mtu aliyekuwa anapigwa huku akiwaambia “mwachieni, mwachieni, namfahamu
mimi huyo ni mwandishi wa habari!”</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Senga
alisema mara alisikia kishindo kikubwa na wale askari ambao walikuwa
wanamshikilia walikimbia ndipo yeye akaendelea kupiga picha sasa za
marehemu Daud Mwangosi ambaye alikuwa amekwisha sambaratishwa na bomu.
Alieleza kuwa alimsikia yule askari ambaye alikuja kumsaidia marehemu
Mwangosi akisema “afande wameniuwa”, “afande wameniuwa”, akimwambia RPC
ambaye alikuwa karibu nae kwani nae aliumizwa vibaya katika mlipuko huo.
Senga aliiambia Kamati wale wote ambao walikuwa wame mzunguka marehemu
kama wanavyoonekana kwenye picha alizopiga walikuwepo wakati anapigwa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Maelezo
ya Bw. Senga yanatofautiana sana na yale yaliyotolewa na RPC na OC FFU
kuwa Marehemu alimvamia OCS Mwampamba na kuwa wale askari huenda
walidhania kuwa mkubwa wao alikuwa amevamiwa ndipo walipoamua kwenda
kumsaidia. OCS Mwampamba mwenyewe wakati akihojiwa na Kamati ilipokuwa
Mafinga alisema hakumbuki kitu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Hata
hivyo, kwa maelezo ya Bw. Senga, ambayo yanakubaliana na yale ya RPC na
OC-FFU, kitendo cha kupigwa na mauaji ya marehemu Daud Mwangosi
kilitokea baada ya kuisha ile operesheni ya kusambaratisha mkutano wa
CHADEMA na hapakuwa na mabishano yeyote au purukushani iliyotokea kabla
ya marehemu kuzungukwa na kuanza kupigwa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa
minajili hii basi Kamati imeshindwa kubaini baada ya kumalizika
operesheni na askari Polisi kuanza kuondoka, kwa nini Mwangosi
alishambuliwa kwa kipigo kabla ya kulipuliwa na bomu la kishindo?</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa
nini kuna maelezo yanayokinzana kati ya Bw. Senga ambaye alikuwa karibu
sana na tukio na yale ya RPC na OC-FFU ambao katika maelezo yao kwa
Kamati walisema kuwa wao walikuwa mbali kidogo na tukio kwa hiyo
hawakuweza kuona kwa dhahiri kilichotokea. Maelezeo ambayo yalirudiwa na
viongozi wa juu wa Polisi ikiwa ni pamoja na Kamishna wa Upelelezi
(DCI) Robert Manumba na Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema katika
mahojiano na Kamati.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Uchunguzi
wa Kamati haukuweza kupata ushahidi wa kubainisha kama kupigwa kwa
waandishi hao kulitokana na njama yeyote ya Polisi kuwashughulikia au
ilitokea kwenye purukushani ya vurugu zilizotokea baada ya FFU kuamriwa
kutawanya wanachama wa CHADEMA.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Pia
Kamati haikupata ushahidi wowote wa kuonyesha kuwa mauaji ya Daud
Mwangosi yalikuwa ni ya kupangwa. Kutokana na maelezo ya hapo juu,
Kamati inapendekeza yafuatayo:-</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Taasisi
za habari zinazosimamia maadili na weledi wa vyombo vya habari, hususan
Baraza la Habari Tanzania na Jukwaa la Wahariri wafanye utaratibu
unaostahiki za upatanishi kati ya waandishi wa habari, Jeshi la Polisi
na uongozi wa mkoa wa Iringa. Hii itasaidia kurejesha uhusiano mzuri
kati ya vyombo hivyo muhimu katika mkoa;</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Waandishi wa habari wapewe mafunzo ya jinsi ya kuripoti matukio ya hatari/ghasia;</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Waandishi wa habari wavae vivazi maalum vya kuwatambulisha wakiwa katika matukio hasa kwenye maeneo hatarishi;</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Waandishi wa habari wafanye kazi kwa weledi, uadilifu, uwazi na wasijibainishe na vyama vya siasa;</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Polisi ambao walihusika katika kumpiga marehemu Daud Mwangosi kabla hajauawa wachukuliwe hatua stahiki za kisheria;</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-
Kamati ya Ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na Waandishi wa Habari
iliyoanzishwa mwaka 2008 ifufuliwe. Na kamati hizo ziteremke hadi kwenye
ngazi ya mkoa kama ilivyokuwa awali.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Viongozi wa polisi wanapotoa taarifa za tukio, ziwe zimefanyiwa utafiti wa kina ili zisipotoshe jamii.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>7.5
Uwepo wa Sheria, Kanuni au Taratibu zinazotoa uwezo kwa Jeshi la Polisi
kuzuia mikusanyiko inayoitishwa na Vyama vya Siasa na Mamlaka ya Rufaa
ambapo Vyama hivyo havitaridhika na amri hiyo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Sheria
Namba 5 ya 1992 kama ilivyorekebishwa na Sheria Namba 7 ya 2009
inaratibu mahusiano ya kiutendaji kati ya Jeshi la Polisi na Vyama vya
Siasa. Kwa mujibu wa Sheria hii Jeshi la Polisi limepewa madaraka ya
kutoa zuio kwa maandishi na kuweka bayana sababu za kuzuia mikutano au
maandamano. Zuio aina hii ni halali kwa mujibu wa Sheria na ni sherti
Chama cha Siasa kiheshimu na kutii. Fungu la 11 vifungu vidogo Na 1, 4,
5, 6, 7 na 8 ya Sheria ya Vyama vya Siasa likisomwa pamoja na mafungu
Namba 43, 44, 45 na 46 ya Sheria ya Jeshi la Polisi na Auxiliary Forces
Act Sura 322 vitatumika kusimamia uendeshaji mikutano ya Vyama vya Siasa
ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong> Pamoja
na kwamba Vyama vya Siasa vinatakiwa kutoa taarifa na siyo kuomba
idhini, Jeshi la Polisi limepewa uwezo na madaraka juu ya mikutano hiyo
kuhusu kuzuia au kuruhusu na au kutoa maelekezo stahiki, kama vile
kupendekeza, na kushauri eneo mbadala na tarehe tofauti ya kufanya
mikutano/maandamano.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Aidha kutotii amri/zuio ya Jeshi la Polisi ni kosa la Jinai kwa mujibu wa Fungu la 74 la Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura 16 RE.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Vilevile
kwa mujibu wa Fungu la 43 (6) ya Sheria ya Jeshi la Polisi na Auxiliary
Forces Act, Waziri wa Mambo ya Ndani ndiye Mamlaka ya Rufaa dhidi ya
amri/zuio linatolewa na Jeshi la Polisi.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Pamoja
na kuwepo kwa Sheria hizi mbili bado kuna mapungufu katika uendeshaji
na usimamizi wa shughuli za Siasa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa. Kwa
mfano pamoja na madaraka aliyonayo Msajili wa Vyama vya Siasa ya
kukifuta Chama cha Siasa kwenye rejesta ya usajili kwa mujibu wa Fungu
la 19 na 20 ya Sheria ya Vyama vya Siasa, kusimamisha utoaji wa ruzuku
na matumizi yake, uratibu wa shughuli za vyama hivyo hauko mikononi
mwake.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Wadau
wanashauri umuhimu wa kuimarisha uhusiano katika shughuli za utendaji
kati ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na Jeshi la Polisi ili
kudumisha utulivu na amani na utii wa sheria bila shuruti kwa upande
mmoja na kukuza mfumo wa Demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa kwa upande
mwingine.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>7.6 Hali ya mahusiano kati ya Jeshi la Polisi na Vyama vya Siasa nchini katika utendaji kazi wao na Utii wa Sheria.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kamati
ya Uchunguzi wa Kifo cha Mwandishi wa Habari wa Channel Ten, Daud
Mwangosi katika kupata majibu kwa hadidu hii ya rejea, ilizungumza na
viongozi wa vyama vya siasa kutoka ngazi za Kijiji cha Nyololo, Wilaya
ya Mufindi, Mkoa wa Iringa na Viongozi wa kitaifa jijini Dar es Salaam
na viongozi wa dini kutoka ngazi za Kijiji cha Nyololo, Wilaya ya
Mufindi na Mkoa wa Iringa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa
ujumla, kila kiongozi wa chama cha siasa wa ngazi zote ambaye Kamati
imezungumza naye kuhusu hadidu hii ya rejea, ameelezea umuhimu wa Jeshi
la Polisi katika kulinda usalama wa raia na mali zao na wangependa jeshi
hilo liachwe huru katika kutekeleza majukumu yake bila ya kuingiliwa na
wanasiasa ili lifanye kazi zake kwa weledi na uadilifu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Hata
hivyo taswira iliyojitokeza ni kwamba kuna mgawanyiko wa mtizamo kuhusu
jinsi Jeshi la Polisi linavyoshughulikia mikutano/maandamano ya Vyama
vya Siasa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Baadhi
ya viongozi wa vyama vya upinzani wanaamini kuwa Jeshi la Polisi
linakipendelea Chama cha Mapinduzi na kubinya vyama vya upinzani, huku
viongozi wa CCM kutoka ngazi ya kijiji hadi Taifa wakilisifia Jeshi hilo
kuwa linafanya kazi yake vizuri na kwa weledi mkubwa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Mgawanyiko
wa taswira kuhusu madai kuwa Jeshi la Polisi kuipendelea CCM hauko tu
kati ya vyama vya upinzani na CCM bali pia kwa viongozi wa dini kuanzia
ngazi za kijiji, wilaya hadi mkoani Iringa kwa maelezo kuwa hawajasikia
hata siku moja mtu anauawa na Polisi kwenye mkutano wa CCM. Mwandishi
mmoja alitoa udadisi wake kuwa huwa wanapata shida sana kuandika habari
za mikutano ya CHADEMA kutokana na jinsi Polisi wanavyojipanga kwenye
mikutano ya chama hicho.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kudhihirisha
umuhimu wa Jeshi la Polisi katika jamii, hata wale wanaolituhumu kuwa
linakipendelea CCM, katika kutoa maoni yao kuhusu hatua za kuchukuliwa
askari wanaoharibu sifa ya Jeshi hilo, wanapendekeza kuwa askari
wahusika wachukuliwe hatua na kuomba Jeshi hilo liendeshwe kwa weledi
hasa inapotokea askari akalazimika kutumia silaha kukabiliana na fujo
isifikie kuua.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa
mfano, Mchungaji Peter Katanga wa Revival Baptist Church, alishauri
chombo cha Polisi kisitumike kufanya mauaji, au kisitumike na mtu, watu,
au kikundi chochote kufanya matendo yasiyo mazuri kwa jamii kwa sababu
chombo hicho kipo kwa ajili ya kulinda usalama wa raia wote na mali zao.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Viongozi
wa siasa wengine bila kujali itikadi zao, wameonekana kukerwa sana na
tabia ya watu kuuawa wakati Jeshi la Polisi linatuliza ghasia na hii
ikiachiwa iendelee inaweza kuleta uvunjifu wa amani katika nchi. Kwa
mfano, Mchungaji wa Kanisa la EFATA Nyololo, Mkombozi Kiliwa alishauri
Polisi watumie njia zinazofaa kukabiliana na wanaovunja sheria na si
kuua.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Pia
Mwalimu wa Shule ya Msingi Nyololo, Obby Kimbale, alielezea
kutokukubaliana kwake na kitendo cha mauaji ya Daud Mwangosi,
alipendekeza elimu ya uraia itolewe kwa jamii nzima vikiwemo vyombo vya
dola, viongozi wa serikali, wanasiasa na wananchi kwa ujumla wao ili
kila mtu kwa nafasi yake akaelewa namna ya kutimiza wajibu wake ndani ya
mfumo wa demokrasia ya vyama vingi.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa
upande mwingine, wengi waliotoa maoni yao juu ya mahusiano ya Polisi na
vyama vya siasa, pamoja na kulaumu Jeshi la Polisi kutumia nguvu kubwa
katika kukabiliana na wafuasi wa CHADEMA, pia waliwalaumu viongozi wa
chama hicho, kwa kutotii amri halali ya Jeshi la Polisi hatimaye
kusababisha Polisi kutumia nguvu kiasi hicho.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kitendo
cha kuuawa kwa Mwandishi wa Habari, Daud Mwangosi na tabia ya kutokea
mauaji katika mikutano ya CHADEMA kimeonekana kuwakera viongozi wengi wa
vyama vya siasa kwani wanaamini kuwa Polisi huwa wanatumia nguvu kubwa
kupita kiasi ‘wanapotuliza ghasia’ katika mikutano ya CHADEMA.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Katibu
wa CCM Wilaya ya Iringa, Zakaria Mwansasu alielezea sababu ya matukio
ya namna hii kuwa ni kutokana na mmomonyoko aliouita mkubwa wa maadili
hasa katika vyama vya siasa na akashauri viongozi wa vyama vya siasa
wakapewa elimu ya uraia.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Maoni
mengi ya viongozi wa vyama vya siasa yamejikita zaidi katika hofu ya
nchi kuingia kwenye vurugu na kutoka kwenye kisiwa cha amani na hivyo
kutoa uashauri kwa viongozi wa vyama vya siasa na Jeshi la Polisi kuweka
mbele maslahi ya taifa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Mchungaji
Yokonia Koko wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT),
alielezea ukosefu wa maadili kwa baadhi ya askari Polisi kuwa umetokana
na jeshi hilo kuajiri vijana ambao hawana maadili na kwamba watuhumiwa
wa mauaji kwenye matukio yanayolihusisha Jeshi la Polisi wakati wa
kuzuia fujo katika mikutano/maandamano ya vyama vya siasa wachukuliwe
hatua kali ili iwe fundisho kwa askari wengine.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kasi
ya CHADEMA kuendesha mikutano katika sehemu mbalimbali nchini kwa ajili
ya kujiimarisha kichama, imepokewa kwa hisia tofauti na vyama vingine
vya siasa. Wakati kuna makundi ya watu katika jamii wakidhani kuwa hiyo
ni haki yao kama chama cha siasa kinachotaka kukua na kukubalika
kisiasa, wengine wanaiona mikutano hiyo ya hadhara ya CHADEMA kama ni
kuwapunguzia muda wa kufanya shughuli zao za maendeleo hasa baada ya
kipindi cha uchaguzi kumalizika.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Katibu
Mkuu wa CCM Wilson Mukama, alishauri kufanyiwa marekebisho kwenye
sheria ya Vyama vya Siasa Namba 5 ya mwaka 1992 itakayoweka wazi
shughuli za vyama vya siasa baada ya Uchaguzi Mkuu. Alisisitiza kuwa
shughuli za siasa baada ya Uchaguzi Mkuu zihamie bungeni kwa wanasiasa
kuhoji mipango ya maendeleo ya serikali na matumizi ya rasilimali za
nchi na wananchi waachwe wachape kazi zao za maendeleo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kuhusu
Jeshi la Polisi, Mukama alisema mfumo uliopo wa Jeshi hilo unalifanya
lionekane la kitaifa zaidi na kushauri libadilishwe kimuundo ili liweze
kutandaa hadi serikali za mitaa kuongeza nguvu katika mpango wa ulinzi
shirikishi ulioanzishwa na Jeshi hilo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Mwanasiasa
John Shibuda alizungumzia mahusiano kati ya vyama vya siasa na Jeshi la
Polisi kwa kutoa lawama kwa vyama vya siasa kuwa havitoi malezi kwa
wanachama wake ambayo yatawafanya wawe waadilifu, wazalendo, waaminifu
na watiifu wa sheria.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Alisema
vyama vya siasa havina mfumo wa kujihakiki, kujikosoa na kujiwajibisha
na akapendekeza kuanzishwa kwa mfumo huo kisheria ambao utawajibisha
vyama vya siasa kwa matendo ya viongozi au wanachama wao.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Shibuda
alifafanua kwamba sheria anayopendekeza iwe na nguvu ya kutoa adhabu
kwa chama cha siasa na kwa kiongozi au mwanachama ambaye atathibitika
kuwa ndiyo chanzo cha uvunjifu wa amani.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kuhusu
Jeshi la Polisi mwanasiasa huyo alipendekeza kufanyike kwa marekebisho
ya utendaji ili wakuu wa wilaya na mikoa waondolewe nguvu za kiutawala
ambazo huwafanya wakati mwingine kutoa maagizo ya kisiasa kwa Jeshi la
Polisi na hatimaye kulifanya Jeshi hilo lionekane linatekeleza maslahi
ya wanasiasa badala ya kuwa chombo cha kulinda amani.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa
ujumla Kamati kutokana na maelezo mbalimbali ya Viongozi wa Vyama vya
Siasa na Jeshi la Polisi, imeona kuwa kuna mahusiano hafifu kati ya
baadhi ya Vyama vya Siasa na Jeshi la Polisi.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kwa kuwa taasisi zote hizi ni wadau muhimu wa amani na utulivu nchini, Kamati inapendekeza:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kuwe
na jukwaa la mazungumzo ya mara kwa mara kati ya Jeshi la Polisi na
Vyama vya Siasa ili kila upande ujue wajibu wake na wa taasisi nyingine
katika kudumisha amani ya nchi na utamaduni wa kuheshimu sheria zilizopo
na kupunguza migongano.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kuhusu
madai kwamba mauaji yanayotokea nchini yaundiwe Tume, Kamati imeona
kuwa zipo sheria zinazotoa mamlaka ya kutafiti au kuchunguza endapo kuna
mashaka ya kifo hicho.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Muundo
uliopo wa Jeshi la Polisi uangaliwe upya kisheria ili kuziba mianya
inayotoa nafasi kwa wanasiasa kulitumia Jeshi hilo kwa manufaa ya
kisiasa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Nafasi za Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa kiutendaji ziangaliwe upya ili zisitumike na mhusika kwa ajili ya manufaa ya kisiasa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kwa
kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kuwa ndiye mlinzi wa usalama wa raia
na mali zao, siasa za ubabe kwa vyama vya siasa ziepukwe kwa kuwa
zinaleta msuguano usio wa lazima na Jeshi la Polisi</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>8.0. MAONI NA MAPENDEKEZO:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kutokana
na uchunguzi uliofanyika kupitia mahojiano na Viongozi wa kada
mbalimbali, kuanzia ngazi ya Kijiji, Wilaya, Mkoa hadi Taifa, Kamati ina
maoni na mapendekezo yafuatayo:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>MAONI:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kuhusu
madai kwamba mauaji yanayotokea nchini yaundiwe tume, Kamati imeona
kuwa zipo sheria zinazotoa mamlaka ya kutafiti au kuchunguza endapo kuna
mashaka ya kifo hicho.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Nafasi za Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa kiutendaji ziangaliwe upya ili zisitumike na mhusika kwa ajili ya manufaa ya kisiasa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kwa
kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kuwa ndiye mlinzi wa usalama wa raia
na mali zao, siasa za ubabe kwa vyama vya siasa ziepukwe kwa kuwa
zinaleta msuguano usio wa lazima na Jeshi la Polisi</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kuhusu
operesheni ya uzuiaji wa mkutano wa CHADEMA usio halali Kijijini
Nyololo tarehe 02 Septemba 2012, Jeshi la Polisi lilitekeleza wajibu
wake ipasavyo na kutumia nguvu sahihi. Operesheni iliyoandaliwa na
kufanyika ilikamilika kwa kuwatawanya watu waliofika kwenye mkutano,
kukamata baadhi ya Viongozi na wafuasi wa CHADEMA na hali ya utulivu
ilirejea kwenye eneo husika.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>MAPENDEKEZO</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Mauaji
ya mwandishi wa habari Daud Mwangosi yalitokea baada ya operesheni
kumalizika, na amri ya kuondoka kwa askari eneo la tukio kutolewa na
Viongozi wa operesheni hiyo</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Jamii
wakiwemo Viongozi waelimishwe umuhimu wa utii wa sheria, kanuni na
taratibu ili kudumisha amani na utulivu hapa nchini. Viongozi wengi
walionyesha hofu ya kuliingiza Taifa kwenye machafuko makubwa na
uvunjifu wa amani iwapo jamii haitazingatia umuhimu wa kutii sheria,
kanuni, taratibu na amri halali za Mamlaka.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Msajili
wa Vyama vya siasa afafanue majukumu ya vikundi vya Ulinzi vya Vyama
vya Siasa kama vile Green Guard, Red Brigade, Blue Guard.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Iwepo
programu mahususi ya Elimu ya Uraia nchini ili kujenga uzalendo na
kukuza maadili ndani ya jamii wakiwemo viongozi wa kada mbalimbali. Hivi
sasa jamii inashuhudia kutoweka kwa uzalendo na kuwepo kwa mmomonyoko
wa maadili ndani ya jamii.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Njia zifuatazo zitumike:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Elimu ya uraia iimarishwe katika mitaala ya elimu kuanzia Shule za msingi hadi Vyuo Vikuu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Uamuzi wa kurudisha mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa vijana utekelezwe mapema.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-
Vyama vya Siasa, Madhehebu ya Dini, Tasnia ya Habari na Taasisi
zisizokuwa za Serikali zishiriki kikamilifu katika uenezi wa Elimu ya
Uraia nchini.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-
Kuhimiza uzingatiaji wa weledi katika utendaji kazi kwa mujibu wa
taaluma na miongozo inayotolewa kuleta ufanisi. Aidha elimu endelevu
sehemu za kazi itiliwe mkazo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kufanya
marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa Na. 5 ya 1992 ili kuweka wazi
shughuli za Vyama vya Siasa baada ya Uchaguzi Mkuu. Lengo ni kuwa
Shughuli za Siasa zihamie Bungeni kujadili na kuhoji mipango ya Serikali
na matumizi ya rasilimali za nchi. Kwa kufanya hivyo wananchi watapata
nafasi kufanya kazi za maendeleo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kuboresha
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, hususan uanzishwaji wa
ofisi ngazi ya Mkoa na Wilaya ili kuratibu ushirikiano/mahusiano baina
ya serikali (Jeshi la Polisi) na Vyama vya Siasa. Lengo ni kukuza
mahusiano na kuondoa mgongano.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Utaratibu
wa kufanya mikutano mara kwa mara kati ya Jeshi la Polisi na Vyama vya
Siasa, Jeshi la Polisi na Waandishi wa Habari uimarishwe ili kujenga
mahusiano mazuri na kupata ufumbuzi wa haraka kwa matatizo
yaliyojitokeza.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-
Jeshi la Polisi nchini ni chombo muhimu katika ulinzi na usalama wa raia
na mali zao. Muundo uliopo wa Jeshi la Polisi uangaliwe upya Kisheria
ili kuziba mianya inayotoa nafasi kwa wanasiasa kulitumia Jeshi hilo kwa
manufaa ya Kisiasa. Aidha mipango ya kuboresha utendaji kazi kitaaluma
iliyopo hivi sasa upewe msukumo stahiki hususan rasilimali watu na
fedha.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-
Wananchi wahamasishwe kushirikiana na Polisi Jamii na Ulinzi shirikishi.
Polis ishirikiane na Serikali za mitaa kufanikisha malengo hayo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-
Jeshi la Polisi liimarishwe ili litekeleze majukumu yake kikamilifu na
kujenga mahusiano sahihi kati yake na Jamii, Vyama vya Siasa, Tasnia ya
Habari na Asasi zisizo za Kiserikali.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Taasisi
za habari zinazosimamia maadili na weledi wa vyombo vya habari, hususan
Baraza la Habari Tanzania na Jukwaa la Wahariri wafanye utaratibu
unaostahiki wa upatanishi kati ya waandishi wa habari, Jeshi la Polisi
na uongozi wa mkoa wa Iringa. Hii itasaidia kurejesha uhusiano mzuri
kati ya vyombo hivyo muhimu katika mkoa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Waandishi wa habari wapewe mafunzo ya jinsi ya kuripoti matukio ya hatari/ghasia.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Waandishi wa habari wavae vivazi maalum vya kuwatambulisha wakiwa katika matukio hasa kwenye maeneo hatarishi.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Waandishi wa habari wafanye kazi kwa weledi, uadilifu, uwazi na wasijibainishe na vyama vya siasa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kamati
ya Ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na Waandishi wa Habari
iliyoanzishwa mwaka 2008 ifufuliwe. Na kamati hizo ziteremke hadi kwenye
ngazi ya mkoa kama ilivyokuwa awali.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Viongozi wa Polisi wanapotoa taarifa za tukio, ziwe zimefanyiwa utafiti wa kina ili zisipotoshe jamii.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kuwe
na jukwaa la mazungumzo ya mara kwa mara kati ya Jeshi la Polisi na
Vyama vya Siasa ili kila upande ujue wajibu wake na wa taasisi nyingine
katika kudumisha amani ya nchi na utamaduni wa kuheshimu sheria zilizopo
na kupunguza migongano.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>9.0. CHANGAMOTO</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Changamoto zilizojitokeza katika Uchunguzi zimegawanyika katika mtiririko ufuatao:-</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>9.1 Jeshi la Polisi:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Ukosefu wa Mafunzo endelevu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Ukosefu wa Uvumilivu katika utekelezaji wa Majukumu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Uelewa mdogo wa Elimu ya Uraia.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Mmomonyoko wa Maadili.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Kukosekana kwa uzalendo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Ukosefu wa Utii wa Sheria, Kanuni na Taratibu</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>9.2 Vyama vya Siasa:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Kukosekana kwa uvumilivu katika kuendesha shughuli za Siasa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>-Kukosekana kwa Elimu ya Uraia</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Uelewa mdogo wa baadhi ya Viongozi wa Vyama kuhusu uendeshaji wa Vyama vya Siasa.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Ukosefu wa Sera/Mwongozo kwa Vyama vya Siasa kuendesha shughuli za Kisiasa baada ya uchaguzi mkuu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Kukosekana kwa Jukwaa linalokutanisha mara kwa mara Vyama vya Siasa na Jeshi la Polisi</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Mmomonyoko wa Maadili.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Suala la Uzalendo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Ukosefu wa Utii wa Sheria, Kanuni na Taratibu</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>9.3 Jamii:</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Elimu ya Uraia.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Mmomonyoko wa Maadili.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Kukosekana kwa uzalendo.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>- Ukosefu wa Utii wa Sheria, Kanuni na Taratibu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>26</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>10 HITIMISHO</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Hayati
Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere wakati wa uhai wake aliwahi kusema
kuwa, “ili nchi iendelee inahitaji vitu vinne ambavyo ni watu, ardhi,
siasa safi na uongozi bora. Watanzania kila mtu mahali pake, tunahitaji
kuwa na siasa safi yenye kujenga ustawi, tija, mshikamano, amani,
maendeleo na afya kwa taifa letu”.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Utulivu
na amani kwa ajili ya mustakabali wa taifa, imekuwa ni kauli mbiu ya
viongozi mbalimbali ambao Kamati hii imepata fursa ya kuzungumzia juu ya
hali ya siasa na mahusiano yaliyopo baina ya Serikali, (Jeshi la
Polisi, Kamati za Ulinzi na Usalama wilaya na mkoa), vyama vya siasa,
viongozi wa dini na wananchi.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Wananchi
na Viongozi wanataka kuona shughuli za siasa ya vyama vingi inaendeshwa
kwa hoja zenye tija badala ya vurugu na utengano. Njia mojawapo ya
kukabiliana na hali hii inayojitokeza ni kujenga uzalendo, maadili mema,
na mshikamano ili Tanzania iendelee kuwa kisiwa cha amani na utulivu.</strong></span></div>
<div style="text-align: center;">
<span style="color: black;"><strong>Kamati hii inashauri na kupendekeza kuwa maoni haya yazingatiwe na kutekelezwa.</strong></span></div>
<span style="color: black;"><strong>Aidha
Kamati imefaidika sana kupata fursa ya kukutana na viongozi mbalimbali
kuanzia kijiji hadi taifa na walitoa ushirikiano wa dhati katika kutoa
mchango wao wa mawazo. Kamati inapenda kutoa shukrani za dhati kwa
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Dkt Emmanuel Nchimbi (Mb) kwa
imani yake kwa wajumbe wa Kamati ya Uchuguzi.</strong></span><br />
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhVV-NoXYYfklL9ygFZp-3_87eb8X17Oj_LdQB-UuP5N5Okn_KAsm5rs91lmb6jhVlkr3LEUINpdR2sKJ_usEOpXQF8bvC9T4-QPF-iy-Njwoq12pfgiX1YqXRs0FbznzOhVRYvK0a9SC78/s1600/Untitled.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="120" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhVV-NoXYYfklL9ygFZp-3_87eb8X17Oj_LdQB-UuP5N5Okn_KAsm5rs91lmb6jhVlkr3LEUINpdR2sKJ_usEOpXQF8bvC9T4-QPF-iy-Njwoq12pfgiX1YqXRs0FbznzOhVRYvK0a9SC78/s320/Untitled.jpg" width="320" /></a></div>
<span style="color: black;"><strong> Source:Mo blog</strong></span>NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-7879650036115922472012-10-09T20:40:00.001+03:002012-10-09T20:47:48.901+03:00<br />
<br />
<span style="color: red;"> SABABU 10 KWANINI SNOOP DOG ANAMKUBALI OBAMA NA SIO ROMNEY!</span><br />
<br />
Ni siku chache zilizopita Snoop Dog alitangaza kubadili jina lake la kisanii kuwa Snoop Lion. Jamaa ambaye jina lake halisi ni Kevin Brodus Jr. anasema hawezi kumpa support Romney kwa sababu anajiona yeye (Romney) ni bora sana na siku zote amekuwa akiwaongelea watu vibaya na kujiona yeye ni mzuri zaidi yao.<br />
Na anampa support Obama kwa sababu anafanya mambo kama yeye.<br />
<br />
Hizi hapa ndio sababu 10 za snoop kumkubali Obama na sababu 10 za kutomkubali Romney<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjd9LXu0dH-P1L8C39dr2Xqm-E1KMcK6rwDnjUNl4ZqVTzpgxUhKoTqD1CuTzCZyx7QzwTrLU1V4w8Uslxa3OAAqIj16KsJOHsIaFso1z2tL82H1jownGMauZj91PhOaWV7UcglQ-tGWwz0/s1600/snoopmittlist10.52.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjd9LXu0dH-P1L8C39dr2Xqm-E1KMcK6rwDnjUNl4ZqVTzpgxUhKoTqD1CuTzCZyx7QzwTrLU1V4w8Uslxa3OAAqIj16KsJOHsIaFso1z2tL82H1jownGMauZj91PhOaWV7UcglQ-tGWwz0/s320/snoopmittlist10.52.jpg" width="320" /></a></div>
<br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-83998401512633348242012-10-01T11:34:00.003+03:002012-10-01T11:45:10.839+03:00<br />
<span style="color: red;">YOUNG JEEZY NA RICK ROSS WATIFUANA BACK STAGE WAKATI WA TUZO ZA BET HIPHOP AWARDS</span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj2MSTwWVn-2B-1U2zL1y7IwANTJ28AcL5kPgDONon8u1Aa9RkOPW_2Wr_vOGtQHZWrJd7dWQqYVgtKnlpC9Hs9OVcbhQ7fCTNyRaWI0IzugYY3kWi2c21K1IiBtVGyib9B9K6CeSSN_y8t/s1600/ross-vs-jeezy.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="216" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj2MSTwWVn-2B-1U2zL1y7IwANTJ28AcL5kPgDONon8u1Aa9RkOPW_2Wr_vOGtQHZWrJd7dWQqYVgtKnlpC9Hs9OVcbhQ7fCTNyRaWI0IzugYY3kWi2c21K1IiBtVGyib9B9K6CeSSN_y8t/s320/ross-vs-jeezy.jpg" width="320" /></a></div>
Kwa mbali unaweza kumwona Rozay aliye kifua wazi na watu wengine pia wanaonekana,hapo ni wakati wa tifu lenyewe.<br />
<br />
<span style="color: red;"> <span style="color: black;">Ilikuwa back stage kwenye tuzo maarufu za BET HIPHOP AWARDS zilizokuwa zinafanyika Atlanta ambapo Rozay na Young Jeezy walianza kurushiana maneno na ghafla kusukumana.</span> <span style="color: black;">Tukio hilo la ajabu lilipelekea risasi kusikika na inaelezwa ni mmoja wa watu wa karibu Rick Ross ndio alirusha risasi. Ingawa inaelezwa kuwa kutoweka huko kwa amani kulifanikiwa kutulizwa na watu wa usalama na shughuli nyingine kuendelea kama kawaida. </span></span><br />
<span style="color: red;"><span style="color: black;"> Ni takribani miaka kama miwili ambapo Young Jeezy na Rick Ross wamekuwa hawaelewani na chanzo kinaelezwa kuwa ni pale Rick Ross alipotoa wimbo wa BMF (Blowing Money Fast) na Young Jeezy kumponda Rick Ross kuwa anaimba asichokijua. Katika wimbo wa BMF rozay anamtaja Big Meech ambaye ni mmoja wa watu wa karibu wa Young Jeezy na kwa sasa yupo jela. Na ndio sababu ya Young Jeezy kumponda Rozay kuimba wimbo unaomuhusu mshikaji wake wa muda mrefu.</span></span><br />
<span style="color: red;"><span style="color: black;">Hivi karibuni Rick ross alieleza kuwa yupo tayari kufanya kazi na Young Jeezy na kulikuwa na tetesi ya uwezekano wa wawili hao kufanya kazi ya pamoja.</span></span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgD-dScoM7DdensJYZ8SxVVl5qehLeZuhWyJJfsrF_p-jscK_ODw_RGCVZk5ybki9Km1xXewH3AW3jHyMg0PUzWBLhhr3m1-Lrui-lNh01XsqcPyplEQklbybyPn4RynADCYBwx4k2nM5z6/s1600/Rick-Ross-Young-Jeezy-scuffle.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="213" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgD-dScoM7DdensJYZ8SxVVl5qehLeZuhWyJJfsrF_p-jscK_ODw_RGCVZk5ybki9Km1xXewH3AW3jHyMg0PUzWBLhhr3m1-Lrui-lNh01XsqcPyplEQklbybyPn4RynADCYBwx4k2nM5z6/s320/Rick-Ross-Young-Jeezy-scuffle.jpg" width="320" /></a></div>
Hapa ni 'long time a go' wakati Rozay na Young Jeezy wakiwa washkaji. Katikati yao ni Jay-z<br />
<span style="color: red;"><span style="color: black;"><br /></span></span>
<span style="color: red;"><span style="color: black;"> </span></span><br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-48393649988850015032012-09-30T02:29:00.000+03:002012-09-30T02:29:37.980+03:00<br />
<span style="color: red;"> AINA GANI YA MSWAKI NI NZURI KWA KUSAFISHA KINYWA NA MENO?</span><br />
<br />
Inaelezwa kuwa, kwa mujibu wa madaktari wengi wa kinywa wanashauri watu kutumia miswaki ambayo kile kichwa au sehemu ya kuswakia iwe ni ndogo na hata iwe laini. Hii itasaidia kinywa kusafishwa kwa urahisi kabisa,na mswaki kufikia maeneo yote yenye uchafu au vijidudu ambavyo ni hatari. Ila kama ni shepu au aina ya mswaki inashauriwa kutumia ule ambao utahisi ni mzuri na unaweza kutumia.<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgAPBOYo0l14qAQ2vma_KTSTiAE_D71iqFCcsMq5D3HsVVcLX-Stkw3uOP72VshW0L_RHrm9d0AtNrcG8pJZn7JneQaj-aWxRhx1vhcRAaBHOfCK_ndBh-w5yRbU4kjYb9Hn5moe9i_rROj/s1600/toothbrushes.jpg" imageanchor="1" style="clear: left; float: left; margin-bottom: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgAPBOYo0l14qAQ2vma_KTSTiAE_D71iqFCcsMq5D3HsVVcLX-Stkw3uOP72VshW0L_RHrm9d0AtNrcG8pJZn7JneQaj-aWxRhx1vhcRAaBHOfCK_ndBh-w5yRbU4kjYb9Hn5moe9i_rROj/s1600/toothbrushes.jpg" /></a></div>
<br />
<span style="color: red;">Je nibadili mswaki kila baada ya muda gani?</span><br />
Unashauriwa kubadili mswaki mara tu unapoona ile sehemu ya kuswakia imeshaanza kuchoka. Lakini ni vizuri zaidi kubadili mswaki kila baada ya miezi 3.<br />
<br />
<br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-40245166276066827012012-09-27T21:05:00.001+03:002012-09-27T21:07:08.992+03:00RICK ROSS KUTUA TANZANIA A.K.A BONGO TAREHE 6 OKTOBA<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjiRBakdIZpZ7lee4tkt25Nl9gxm07aKzLB1D1KxcSFPpTfmZQfSCh4-ET4PjsSJQCGAmMRSHvOva-udZKVLFlyA8YeMBFAoWwYdIq2LcANnzoTPo8PSWR6TonIZQ1iZtps6a2Tn3LkwkRi/s1600/Rick-Ross-Motorcycle.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="213" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjiRBakdIZpZ7lee4tkt25Nl9gxm07aKzLB1D1KxcSFPpTfmZQfSCh4-ET4PjsSJQCGAmMRSHvOva-udZKVLFlyA8YeMBFAoWwYdIq2LcANnzoTPo8PSWR6TonIZQ1iZtps6a2Tn3LkwkRi/s320/Rick-Ross-Motorcycle.jpg" width="320" /></a></div>
Rapper bilionea kutoka USA William Robert a.k.a Rick Ross anatarajia kupiga show nchini Tanzania tarehe 6 mwezi oktoba. Rapper huyo ambae album yake aliyoachia tarehe 31 july imefanikiwa kushika namba moja katika chati za muziki zenye kuheshimika za Billiboard. Ni miongoni mwa wasanii wa marekani wenye kutajwa kuwa na mafanikio katika upande wa muziki na biashara. Rick Ross anamiliki kampuni ya muziki ya Maybach Music Group ambayo inamkataba na Kampuni ya Warner Bross Music Group ambao Roza aliwahi kueleza wakati fulani kuwa ni mkataba wenye thamani ya dola za marekani milioni 25. Huku akiwa ndio CEO wa MayBach Music Group ambayo inasimamia wasanii maarufu akiwemo Meek Mill,Wale,French Montana,Rockie Fresh na wengine kibao.<br />
Pia Rick Ross ana miliki mgahawa wa Boss Wings ambayo ni sehemu ya migahawa maarufu duniani ya Wing Stop. Wakati huo huo akiwa na mikataba kibao ikiwemo na kampuni ya Reebok,Ciroc vodka na kadhalika.<br />
Katika jarida la forbes mwaka huu alitajwa kama miongoni mwa wasanii 20 waliotengeneza pesa nyingi kuanzia mwaka jana hadi mwaka huu.<br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-73534591287395499832012-09-25T12:01:00.002+03:002012-09-25T12:01:41.217+03:00<br />
<br />
<div style="color: red;">
UMESHATAZAMA VIDEO YA HOLD ME BACK YA RICKROSS ALIYOFANYA NIGERIA?</div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
</div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<br /><iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/xu60JoFAN78?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe></div>
<div style="color: red;">
<span style="color: black;">Hopefully umeshatazama video mpya ya Rick Ross ambayo ameirudia kuifanya kule nchini Nigeria,kama ujaiona basi hipo hapo juu. Baadhi ya watu wamelalamika kuwa video hii inajaribu kuionyesha Afrika ni mahala pabaya na watu ni maskini sana. Na hii ni kwasababu kuna vipande katika video inaonekana watoto wadogo wakipewa pesa na hata baadhi ya sehemu kunaonekana watu wakiwa wamevaa nguo chakavu...yaani kwa ufupi watu maskini na maeneo maskini ndio vitu vinavyoonekana zaidi. </span></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/HVO5WhIm4uI?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe></div>
<div style="color: red;">
</div>
<div style="color: red;">
<span style="color: black;">Wakati huo huo watu wengine wanasema Rozay amejaribu kuionesha dunia ukweli wa hali halisi ya Afrika...</span></div>
<div style="color: red;">
<span style="color: black;">Kama ungepata nafasi ya kuiona video nyingine ( First version) ambayo ameifanya USA ambayo ameifanyia New Orleans pia amejaribu kuonesha maeneo chakavu na watu maskini.</span></div>
<div style="color: red;">
<span style="color: black;">Nini maoni yako katika hili?</span></div>
<div style="color: red;">
<span style="color: black;"> </span></div>
NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-54190886197927903612012-09-16T22:46:00.000+03:002012-09-16T23:05:39.555+03:00 <br />
<br />
<div style="color: red;">
<span style="font-size: large;"> BAKHRESSA MMOJA WA MATRILIONEA WAKUBWA AFRICA.</span></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgT-IbclnSEvhq-D6nEFlfaF5K4QMGOW_Q9QqB8biTNiXNDzxlZOfxz1bpkUeAqdzp_YtwjWH4YPtSZ_HghTahJPXGCBqP2mY5e6aRk4iRTplLuRMIN4CJyAU0uNr7mGB0j6JgFmiK8Fq-9/s1600/GO9G5020.JPG" imageanchor="1" style="clear: left; float: left; margin-bottom: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgT-IbclnSEvhq-D6nEFlfaF5K4QMGOW_Q9QqB8biTNiXNDzxlZOfxz1bpkUeAqdzp_YtwjWH4YPtSZ_HghTahJPXGCBqP2mY5e6aRk4iRTplLuRMIN4CJyAU0uNr7mGB0j6JgFmiK8Fq-9/s320/GO9G5020.JPG" width="62" /></a></div>
<br />
<br />
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;">Kwa mujibu wa jarida maarufu duniani,Said Salim Bakhressa ni miongoni mwa matajiri wakubwa Africa ambao utajiri wao unaongezeka kwa kasi. Kwa mujibu Forbes Magazine Kampuni yakeya Bakhressa Group inatengeneza mauzo yanayohfikia dola za marekani milioni 800 sawa na shilingi za Tanzania trilioni 1.2.</span></span><br />
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;">Kama ukipata nafasi ya kujua au kusimuliwa namna mzee huyu alivyoanza inaweza ikakushangaza lakini pia ikakupa nguvu. Kwani wahenga wanasema ''polepole ndio mwendo''. Mzee alianza na kuuza viazi na baadae alifungua migahawa. </span></span><br />
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;">Hii ni changamoto na inspiration kwa vijana wenzangu. Ninachoamini ni kuwa ukifanya kile unacokipenda na ukakifanya kwa moyo wote na bidii yote utafanikiwa.</span></span><br />
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;">Nakumbuka Mama yangu aliponiambia kuwa wakati nikiwa mtoto mdogo kwenye miaka ya themanini mwishoni na tisini mwanzoni alipokuwa ananipeleka hospitali ya Muhimbili tulikuwa tunakula kwenye migahawa yake. Na sasa nimekuwa mkubwa kabisa bado ninakunywa na kutumia bidhaa ambazo amebuni. </span></span><br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-22520575729617882872012-09-12T10:38:00.002+03:002012-09-12T10:38:34.732+03:00 <br />
<span style="font-size: large;"> <span style="color: red;"> TUTAZAME 'BEHIND THE SCENE' ZA KUSISIMUA</span></span><br />
<br />
<span style="font-size: large;"><span style="color: red;"><span style="color: black;"><span style="font-size: small;"> Kwanza wengi wetu tunalipenda lile tangazo la Epic Bongo Star search ambalo linasisimua wengi kutokana na namna lilivyotengenezwa.</span></span></span></span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/l0qiwp8seFs?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe></div>
<span style="font-size: large;"><span style="color: red;"><span style="color: black;"><span style="font-size: small;"> Hilo hapo juu umeliona? Eeeh!!</span></span></span></span><br />
<br />
<span style="font-size: large;"><span style="color: red;"><span style="color: black;"><span style="font-size: small;">Sasa hapa chini ndivyo ambavyo lilitengenezwa</span></span></span></span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/xRSG9l3POm0?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe></div>
<span style="font-size: large;"><span style="color: red;"><span style="color: black;"><span style="font-size: small;"> Tazama maubunifu hayo,nilichogundua kumbe limetengenezwa India.</span></span> </span></span>NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-21589783859626710522012-09-12T10:30:00.001+03:002012-09-12T10:30:46.647+03:00<br />
<br />
<span style="font-size: large;">TUTAZAME VIDEO MPYA ZILIZOTOKA MWEZI HUU!!</span><br />
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/VgOKrc3QrpY?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe></div>
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;"> Artist: Ommy Dimpoz</span></span><br />
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;"> Song: Baadae</span></span><br />
<br />
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/vdrqA93sW-8?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe></div>
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;"> Artist: Nicki Minaj</span></span><br />
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;"> Song: Pound the alarm</span></span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/6mz0LQzbQ7k?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe></div>
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;"> Artist: Dully sykes</span></span><br />
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;"> song: Mtoto wa kariakoo</span></span><br />
<br />
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/8bsZs26IExM?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe> </div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<br /></div>
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;"> Artist: Fat Joe ft. Kanye West and Ashanti</span></span><br />
<span style="font-size: large;"><span style="font-size: small;"> Song: Pride and Joy </span> </span>NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-36432398883661971412012-09-11T11:15:00.002+03:002012-09-11T11:15:42.690+03:00 <br />
<div style="color: red;">
<br /> MATANGAZO HAYA YANA ISHARA GANI KWA TAIFA HILI LETU</div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgtKwUfdcG_dB0czK_q-lBuZBxPRCJQT-5cxeK7rDgSP8pziyUEVHGKnRdYP3O2GMPImEoki-stpt4XkWiiHdRIB9hJkm2AGjXFRYYKPSF1CzAM8__-YulkcaeyFCKxTIVlozX6vKPCOr2t/s1600/010.JPG" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="240" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgtKwUfdcG_dB0czK_q-lBuZBxPRCJQT-5cxeK7rDgSP8pziyUEVHGKnRdYP3O2GMPImEoki-stpt4XkWiiHdRIB9hJkm2AGjXFRYYKPSF1CzAM8__-YulkcaeyFCKxTIVlozX6vKPCOr2t/s320/010.JPG" width="320" /></a></div>
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhOTMGaXw8dMh0MfTR2tEe4hAK7sIcXkks7puiS2x9v7a_uoc7xfjDvSH6NTxwt5rJ9wxSODqY1Xit4RWyV67p1B-53W4X6iYHL33rVhl-Bql7kmbPnvND373kPPs6i5LDQGOYY81F_AfC6/s1600/011.JPG" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="240" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhOTMGaXw8dMh0MfTR2tEe4hAK7sIcXkks7puiS2x9v7a_uoc7xfjDvSH6NTxwt5rJ9wxSODqY1Xit4RWyV67p1B-53W4X6iYHL33rVhl-Bql7kmbPnvND373kPPs6i5LDQGOYY81F_AfC6/s320/011.JPG" width="320" /></a></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgpOVD73LoacUmo2eo9E1EK-WL8vzcsuT54AjX10Lon9jvZCHvBecknfQ_39cKanS2qRW7md18YVBSV0-H8DEB7AmBvmkSgp9sQTKJV2p3rxLFlfFjqwLKRQTKayIrMjgpoKorneCw63JNk/s1600/552070_377760568961165_817557693_n.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgpOVD73LoacUmo2eo9E1EK-WL8vzcsuT54AjX10Lon9jvZCHvBecknfQ_39cKanS2qRW7md18YVBSV0-H8DEB7AmBvmkSgp9sQTKJV2p3rxLFlfFjqwLKRQTKayIrMjgpoKorneCw63JNk/s320/552070_377760568961165_817557693_n.jpg" width="320" /></a></div>
<br />
Sasa hivi ukipita sehemu nyingi za mijini utakuta matangazo kama hayo yanayohusu waganga wa kienyeji na ukitazama sifa za waganga hao utagundua kuwa wengi uwa wanataja kutokea miji kama Sumbawanga,Tanga na nchi kama Malawi na Nigeria. Na magonjwa au matatizo makubwa wanayotibu ni nguvu za kiume,matatizo ya uzazi na kazi na mapenzi.<br />
Kingine cha ajabu sasa matangazo hayo mengi uwa yanawekwa kwenye nguzo za umeme.NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-34593110169712279442012-09-10T13:09:00.003+03:002012-09-10T13:09:43.795+03:00 <br />
<div style="color: red;">
<span style="font-size: large;"> SHE IS THE FUTURE HOT TOPIC</span></div>
<div style="color: red;">
<br /></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEirC2pxtGFvua8lV_Ip2ui63qBEQ2LXO_q463UQ4RYndBG3Pl4N41Sekl3HttUYPprWNAjtjfPbyU7tuM6RfwxikYOGRStmYrDG3asqc-Zm1500o6eJ8rOQMZaNt0-bPrHZjL061sH9MO7I/s1600/stella_mwangi_655539p.jpeg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="210" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEirC2pxtGFvua8lV_Ip2ui63qBEQ2LXO_q463UQ4RYndBG3Pl4N41Sekl3HttUYPprWNAjtjfPbyU7tuM6RfwxikYOGRStmYrDG3asqc-Zm1500o6eJ8rOQMZaNt0-bPrHZjL061sH9MO7I/s400/stella_mwangi_655539p.jpeg" width="400" /></a></div>
<br />
Unajua namzungumzia nani? Sio mwingine bali ni Stella Mwangi,binti kutoka kwa mzee Kibaki yaani hapo Kenya,kama umebahatika kutazama au kusikiliza nyimbo zake mbili au tatu utakubaliana na mimi.<br />
Kama vipi,nakupa nafasi utazame video zake mbili za 'Haba haba' na hii ambayo ameitoa hivi karibuni ya 'Bad as i wanna be'. Binti anaonekana analitafuta soko la kimataifa kwa nguvu zote.<br />
<br />
<br />
<br />
<span style="font-size: large;"> <span style="color: black; font-size: small;"> Stella Mwangi- Haba haba (live version</span></span><span style="color: black;">)</span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/o7W-ko3Bbt8?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe> </div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<br /></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
Stella Mwangi-Bad as i wanna be</div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/v5UJp5KMFSc?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe></div>
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-23785584010242617082012-09-03T11:22:00.000+03:002012-09-03T11:22:10.530+03:00 <br />
<span style="color: red;"> NINI MAKOSA YAKE HUYU MWANDISHI WA HABARI?</span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhtVvH3lzLSerirwI8M0KWnuyfZkLvHVJRQ3Fix4d-DYGKc5uKbZo0ZJNVz1L0Jdq28XTDoeOXKbaxUq1KYLBo4WPO9YOD6iy2FHcu6g8VU9tr1U-U9NxeqJBbJxeTPco9WE20IzjVIC2P4/s1600/849116793.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhtVvH3lzLSerirwI8M0KWnuyfZkLvHVJRQ3Fix4d-DYGKc5uKbZo0ZJNVz1L0Jdq28XTDoeOXKbaxUq1KYLBo4WPO9YOD6iy2FHcu6g8VU9tr1U-U9NxeqJBbJxeTPco9WE20IzjVIC2P4/s320/849116793.jpg" width="318" /></a></div>
Anakumbana na mauti tena ya kinyama wakati akiwa kazini,je ni lipi kosa lake?<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgrUlg7-RTzyX7Ne25elhOcqho_LLytdXbPL9VwGzlH5b3AP34FRiZlaPpShVbz-ojp4yynudBE1RtMNYIQHUZMEoh7x8JkchiyQ0o544flbuTxjW_uYmVWKFzjq2sw1CmVXA7b8AMnPDzy/s1600/walivyomwua-wangosi.JPG" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="223" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgrUlg7-RTzyX7Ne25elhOcqho_LLytdXbPL9VwGzlH5b3AP34FRiZlaPpShVbz-ojp4yynudBE1RtMNYIQHUZMEoh7x8JkchiyQ0o544flbuTxjW_uYmVWKFzjq2sw1CmVXA7b8AMnPDzy/s320/walivyomwua-wangosi.JPG" width="320" /></a></div>
Ukitazama vizuri utaona kuwa Bw. Daudi akiwa amemkumbatia mmoja wa maaskari na inavyoonekana alikuwa anapigwa na askari wengine huku huyo askari aliyemkumbatia akionekana kuwazuia wengine kutoendelea kumshambulia. Na hapo hapo kuna askari mwingine mbele yake akiwa ameshika bunduki.<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXvVQDnrrE6yGrs7RPiVL5iWfO29JKKNgpBDtq48U96zRV7-l2B2PwMlI0jIIHLM5lymaVxE0dfivA-y5Zra497E_taM2HLDbfYaFDOBuJpbDl2ZgsoyWG_1VmhDl-GasXhivbMxFBGBBx/s1600/meeting.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="319" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXvVQDnrrE6yGrs7RPiVL5iWfO29JKKNgpBDtq48U96zRV7-l2B2PwMlI0jIIHLM5lymaVxE0dfivA-y5Zra497E_taM2HLDbfYaFDOBuJpbDl2ZgsoyWG_1VmhDl-GasXhivbMxFBGBBx/s320/meeting.jpg" width="320" /></a></div>
Hapa kwa mujibu wa mashuhuda na vyombo vingine vya habari,hapa ilikuwa ni kiasi cha dakika zisizozidi 20 wakati akiwa kazini na kamera yake akiendelea kuchukua matukio kadhaa yaliyokuwa yakiendelea.<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiYJIxMeZvNItdF5JgdlwcB-NdfFEccmye0DFAaY-h2zTCCuaJ8FngY4-5SViMt9GmQKD8keq0uszNgyM5aCibiiwfdM8D-OPGMJQgwlWV3FFelipPdg-xOcFNyIp17O9VyDJsS6tJtiF48/s1600/wanahangaikia-mwenzao-tu.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="239" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiYJIxMeZvNItdF5JgdlwcB-NdfFEccmye0DFAaY-h2zTCCuaJ8FngY4-5SViMt9GmQKD8keq0uszNgyM5aCibiiwfdM8D-OPGMJQgwlWV3FFelipPdg-xOcFNyIp17O9VyDJsS6tJtiF48/s320/wanahangaikia-mwenzao-tu.jpg" width="320" /></a></div>
Sasa je kama ni mlipuko,huo mlipuko ulimpata yeye tu ukawakosa askari wengine? Na kama uliwakosa Askari wengine mbona kuna picha inaonekana alikuwa amemkumbatia askari mwingine na askari huyo akionekana kama anamwokoa na wakati huo huo kuna askari mwingine akiwa ameshika bunduki.<br />
Tazama vizuroi hii picha hapa chini.<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgrUlg7-RTzyX7Ne25elhOcqho_LLytdXbPL9VwGzlH5b3AP34FRiZlaPpShVbz-ojp4yynudBE1RtMNYIQHUZMEoh7x8JkchiyQ0o544flbuTxjW_uYmVWKFzjq2sw1CmVXA7b8AMnPDzy/s1600/walivyomwua-wangosi.JPG" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="223" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgrUlg7-RTzyX7Ne25elhOcqho_LLytdXbPL9VwGzlH5b3AP34FRiZlaPpShVbz-ojp4yynudBE1RtMNYIQHUZMEoh7x8JkchiyQ0o544flbuTxjW_uYmVWKFzjq2sw1CmVXA7b8AMnPDzy/s320/walivyomwua-wangosi.JPG" width="320" /></a></div>
Kwa fikra za kawaida tu,sitaki kusimama upande wowote iwe ni serikali,wananchi au Chama cha CHADEMA. Kinachoumiza zaidi ni kuwa huyu mwandishi wa habari alikuwa kazini.<br />
JE HUYU MWANDISHI ALIKUWA ANA MAKOSA GANI?<br />
<br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-69598069969229638062012-08-29T21:58:00.001+03:002012-08-29T21:58:38.917+03:00<br />
<span style="font-size: large;"><span style="color: red;">KILICHOTOKEA MOMBASA KISITOKEE TENA MOMBASA WALA PENGINE POPOTE</span></span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi1Lz_qyduzPKTrcJrJGKalJDglXbrRPsCZT6qiZi9PmpUc1z6W95zDj1d4EcmMVVHRTqXDBbPSkW-bjJFgXeUMFeE6OFsElaaKXCBxPjwzivUWk1Tr315O0dGHyjDuZkG6cw8F3yYh3tHM/s1600/Sheikh-Aboud-Rogo-shot-dead.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="192" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi1Lz_qyduzPKTrcJrJGKalJDglXbrRPsCZT6qiZi9PmpUc1z6W95zDj1d4EcmMVVHRTqXDBbPSkW-bjJFgXeUMFeE6OFsElaaKXCBxPjwzivUWk1Tr315O0dGHyjDuZkG6cw8F3yYh3tHM/s320/Sheikh-Aboud-Rogo-shot-dead.jpg" width="320" /></a></div>
<br />
<br />
Sheikh Aboud Rogo alikuwa shujaa na role model kwa wengine lakini pia alikuwa adui kwa wengine. Ninalazimika kusema hivyo,na si kwa ubaya bali kwa wema. tukio la mauaji yake limenisikitisha sana.<br />
Naweza nikasema ni mauaji ya kinyama ambayo usingetegemea!Ni tukio lililotokea tena mbele ya familia yake. Kama ilivyosikika katika vyombo mbalimbali vya habari kuwa Sheikh Aboud Rogo alikuwa anampeleka mkewe hospitali na alikuwa kwenye gari pamoja na baba mkwe wake na mtoto wake.<br />
Nimelazimika kusema Sheikh Aboud Rogo alikuwa adui na shujaa kwa watu wawili tofauti kwa sababu;<br />
Inajulikana wazi alikuwa anachukiwa na Marekani kutokana na kumtuhumu kujihusisha na kundi la Al-shabab la Somalia. Lakini pia nalazimika kusema pia alikuwa ni shujaa kwa watu wengine hususani baadhi ya Waislamu.<br />
Sasa baada ya kifo chake tumeshuhudia makanisa yakichomwa,magari ya serikali pia yakichomwa.<br />
SOTE NI NDUGU TOFAUTI ZETU ZA KIDINI ZISITUSABABISHE TUKACHUKIANA AU TUKAJIONA NI BORA ZAIDI YA WENGINE.<br />
Mombasa ni jiji lililopo karibu na Tanga Tanzania na kinachotokea Mombasa kinatuhusu sisi pia Watanzania sio kwa sababu Mombasa ni jirani zetu bali pia tuna mahusiano ya karibu sana,kibiashara na hata kindugu kwani kuna watu wameolewa na kuoa Mombasa. <br />
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
</div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
</div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjAVGCc-leB0ewppPh6BdfZZB1VsJ3nn7LwrRzjnZaRAUJQ25Z0M6Q447sG8gB1Tnv6u0-ENOCYf0rELkZWXH_SQguWFuNUJ1rGiVjBb1c1ByoNFZ_QvNWjQTK0IU8EFq3mEmZItysGDX29/s1600/aboud_rogo.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="204" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjAVGCc-leB0ewppPh6BdfZZB1VsJ3nn7LwrRzjnZaRAUJQ25Z0M6Q447sG8gB1Tnv6u0-ENOCYf0rELkZWXH_SQguWFuNUJ1rGiVjBb1c1ByoNFZ_QvNWjQTK0IU8EFq3mEmZItysGDX29/s320/aboud_rogo.jpg" width="320" /></a></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgKGTxY6Wxs244XTSC39w5nKONPx-a5FVsCkMxkUMcn33VHUd54IbmPIyeI710nXDzEwK-whNnkQaweTky4lvq2IBW1bP1ib1PTMvb-XrPjlTbdlX6q5IHQHYT1yzzFE_DQoDXiuMn4JMfn/s1600/137953284.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="211" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgKGTxY6Wxs244XTSC39w5nKONPx-a5FVsCkMxkUMcn33VHUd54IbmPIyeI710nXDzEwK-whNnkQaweTky4lvq2IBW1bP1ib1PTMvb-XrPjlTbdlX6q5IHQHYT1yzzFE_DQoDXiuMn4JMfn/s320/137953284.jpg" width="320" /></a></div>
Hapo ni enzi za uhai wake<br />
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg2BL5pex9cFgOwmc0f8u81QudrRH4cL58wNlXRqAqv6qKKFR5B0aEtjGFJe5SvUWYAmeTzaFNKpAMa-SRQkmuej5thz5FPqduPgFIH8yfjxpcz6IrnUWXgxzGfgkAZT5c5BFqjfNkazxUz/s1600/Sheikh-Aboud-Rogo-shot-dead.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="192" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg2BL5pex9cFgOwmc0f8u81QudrRH4cL58wNlXRqAqv6qKKFR5B0aEtjGFJe5SvUWYAmeTzaFNKpAMa-SRQkmuej5thz5FPqduPgFIH8yfjxpcz6IrnUWXgxzGfgkAZT5c5BFqjfNkazxUz/s320/Sheikh-Aboud-Rogo-shot-dead.jpg" width="320" /></a></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgcHNSo3NbTqLa_WAW-kTGgB6z7voubTek4XgHCiLCPwxavJMgFMLtxjaaQuyrMcnu2NH4CSIt-R9aY2EVuKJFQMPmvw18QlIDupyzdoO2H117QLfnMjywOSAQ95iItAKmbKm_tXz9FYmq1/s1600/p1d.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="214" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgcHNSo3NbTqLa_WAW-kTGgB6z7voubTek4XgHCiLCPwxavJMgFMLtxjaaQuyrMcnu2NH4CSIt-R9aY2EVuKJFQMPmvw18QlIDupyzdoO2H117QLfnMjywOSAQ95iItAKmbKm_tXz9FYmq1/s320/p1d.jpg" width="320" /></a></div>
Baada ya kifo chake......Ebu tazama huyo mtoto anavyolia,unafikiri hiyo taswira inaweza kupotea akilini mwake kwa muda mfupi?..........<br />
<br />
LET US PRAY FOR THE PEACE OF EAST AFRICA<br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-18560848846280051062012-08-27T12:31:00.001+03:002012-08-27T12:31:29.236+03:00<br />
<br />
<span style="color: red;"> MCHUNGAJI MTOTO EZEKIEL STODDARD ANA MIAKA 11 NA ANAONGOZA KANISA</span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEimsOyCbBQ01Sy3oyB6emlVmwIiryvC1IEXVfm9Gd-veTwvrupHECcMHwdkIs_VMBdBlEO2gRKNz7kj4_TT1NlY9NUzHUwm1eBFic4rvUFKUXQowgikmGoym9C3JAKiLw5PM9flJNFp4blk/s1600/rev-ezekiel-stoddard-PREACH.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="166" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEimsOyCbBQ01Sy3oyB6emlVmwIiryvC1IEXVfm9Gd-veTwvrupHECcMHwdkIs_VMBdBlEO2gRKNz7kj4_TT1NlY9NUzHUwm1eBFic4rvUFKUXQowgikmGoym9C3JAKiLw5PM9flJNFp4blk/s320/rev-ezekiel-stoddard-PREACH.jpg" width="320" /></a></div>
<br />
<br />
<br />
Ana miaka 11 tu lakini ameshaanza kuwashangaza watu wengi kutokana na jinsi anavyohubiri neno la Mungu. Ezekiel Stoddard mtoto anayedai kuwa alipata wito wa kumtumikia Mungu miaka miwili iliyopita. Na ilipofika may mwaka huu akawekwa wakfu kuwa mtumishi wa Mungu katika kanisa la Fulliness of Time huko Maryland Marekani. Wazazi wake wote ni wachungaji wa kanisa hilo. Mtoto Ezekiel anasema ingawa watoto wenzake wamekuwa wakimdhiaki kwamba yeye ni fake pastor lakini uwa hajali hayo yote,bali anasonga mbele.<br />
Ezekiel anasema Mungu alimtokea kwenye ndoto na kumwambia asome Zaburi ya 23. Na alipewa Zaburi<br />
hiyo ili iwe kama muongozo wake. Anasema yeye ni mpenzi wa basketball na tennis na pia anapenda kutazama sinema.<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg1gKjw-p0aJXJQZLAyk3JLsVQEnJOIT7iXg1HenUC5Kq308pCTJLpFn-I2-HD9jsIqkKm9YhMh6WQo2z4mUIJyyRk7ApJjxQF5ptCniJU1ZhZvMcx8O_gLh7V50A762b6vLy-SQF714BtP/s1600/childpreacher26_1339773600.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="217" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg1gKjw-p0aJXJQZLAyk3JLsVQEnJOIT7iXg1HenUC5Kq308pCTJLpFn-I2-HD9jsIqkKm9YhMh6WQo2z4mUIJyyRk7ApJjxQF5ptCniJU1ZhZvMcx8O_gLh7V50A762b6vLy-SQF714BtP/s320/childpreacher26_1339773600.jpg" width="320" /></a></div>
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-62274452267412992312012-08-27T11:40:00.001+03:002012-08-27T11:40:40.251+03:00<br />
<br />
<span style="color: red;">RICK ROSS AKIWA NIGERIA HIVI KARIBUNI!!</span><br />
<span style="color: red;"> </span><br />
<span style="color: red;"><span style="color: black;">Teflon Don a.k.a The Boss hivi karibuni alikuwa nchini Nigeria kuonesha upendo wa Maybach Music au MMG kama wengi wanavyopenda kutamka.</span></span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgg_vLUAtgbbAmxpEiCqUR4mizwD1CaAXm6YfMDbQrZ3MXmfD3wzlZW2LQT8KZ3VIvglwfSrzJcHzXcayrvyOKPqJquIyGOrk_Vg0fE57eM01aYnuOTaDgnQykRRs3HmUsSfGemVk2zxRj9/s1600/ROZAY+IN+NAIJA.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="248" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgg_vLUAtgbbAmxpEiCqUR4mizwD1CaAXm6YfMDbQrZ3MXmfD3wzlZW2LQT8KZ3VIvglwfSrzJcHzXcayrvyOKPqJquIyGOrk_Vg0fE57eM01aYnuOTaDgnQykRRs3HmUsSfGemVk2zxRj9/s320/ROZAY+IN+NAIJA.jpg" width="320" /></a></div>
Hapa akiwa amesongwa na watu kibao...<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
</div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifOJVH84ev-PY_AQIhsw5RyTMvfEpVkyurd2HoQh3VTzdoAOsewjRvjJkrS3zmVRahHMgtJd9wfUIIzbAG750ppR9w6Gk2U7fmThsWcREfy9A3P_Ax_UhI8IfQyC2aRm5WCmw3FoArnjbd/s1600/364081_rick_rosss_jpgf154e6e98b6607db5e47518f4d2fd223.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="240" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifOJVH84ev-PY_AQIhsw5RyTMvfEpVkyurd2HoQh3VTzdoAOsewjRvjJkrS3zmVRahHMgtJd9wfUIIzbAG750ppR9w6Gk2U7fmThsWcREfy9A3P_Ax_UhI8IfQyC2aRm5WCmw3FoArnjbd/s320/364081_rick_rosss_jpgf154e6e98b6607db5e47518f4d2fd223.jpg" width="320" /></a></div>
<br />
<span style="color: red;"><span style="color: black;"> Hapa akiwa anatazama swaga za mtoto wa Naija...</span></span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgE2zhLnEXR_mEZmCrg-AkhPyxwBAvEOQMm5fiyjlccYToDNK1BgCPg7sTQkjqiPlDFrmMwZQQkYqDq6XvEaP6J65ImHK7G2nT1Kw7XYcSzpnFBz5n6TDaWYJx9fWoPupm940YyIWIP-kCc/s1600/341325215.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgE2zhLnEXR_mEZmCrg-AkhPyxwBAvEOQMm5fiyjlccYToDNK1BgCPg7sTQkjqiPlDFrmMwZQQkYqDq6XvEaP6J65ImHK7G2nT1Kw7XYcSzpnFBz5n6TDaWYJx9fWoPupm940YyIWIP-kCc/s320/341325215.jpg" width="320" /></a></div>
<br />
<span style="color: red;"><span style="color: black;"> Takribani miezi michache iliyopita Rozay alifanya bonge la kolabo na wakali 2 kutoka Naija....Paul na Peter ambao wanaunda kundi la P-Square. Ambapo inaelezwa,ingawa haijathibitishwa kuwa P-Square walimlipa kiasi cha dola za marekani laki moja ili tu kufanya naye kollabo.</span></span><br />
<span style="color: red;"><span style="color: black;">Kama ni mfuatiliaji wa You tube utaweza kuona video ya P-Square na Rick Ross imetazamwa na watu zaidi ya millioni nne,kiasi ambacho kwa bara letu la Afrika ni kikubwa sana.</span></span><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQqpUXLaQpQFnJsJmngeQ061q2Qamy8JvvAILnBRe6Dy-rrYajOJjAe6YhTO9zQlWLidYpTwIWUE4lhlb_jIT1cuDKA16lq5sEQ8sQCY8Wn8wacirnH6xRFTXy8UbvlA1AwXI2Bb1j-r9K/s1600/PsquareAkonSLide.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="205" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQqpUXLaQpQFnJsJmngeQ061q2Qamy8JvvAILnBRe6Dy-rrYajOJjAe6YhTO9zQlWLidYpTwIWUE4lhlb_jIT1cuDKA16lq5sEQ8sQCY8Wn8wacirnH6xRFTXy8UbvlA1AwXI2Bb1j-r9K/s320/PsquareAkonSLide.jpg" width="320" /></a></div>
''number one in the game and we gonna be here''<br /><span style="color: red;"><span style="color: black;"> </span></span><br />
<br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-36373608273014723482012-08-23T14:03:00.003+03:002012-08-23T14:03:57.933+03:00<span style="font-size: small;"><br /></span>
<div style="color: red;">
<span style="font-size: large;">JE UNAYAFAHAMU MADHARA YA KUTUMIA DEODORANTS?</span></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg6l7NBQ28HjVjhkfJXv3pknXMgraUoAsp9fHtMPtiLDsYZ21ywRarW3FQ4NLWn3Nu3G-DM3Q7l-_B9FACBQowZoys6kF5H_JfmyAA_tvargk5lRM0-BuL66OTORGvwAgFWHQe5hVE3wPhv/s1600/Deo-women.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg6l7NBQ28HjVjhkfJXv3pknXMgraUoAsp9fHtMPtiLDsYZ21ywRarW3FQ4NLWn3Nu3G-DM3Q7l-_B9FACBQowZoys6kF5H_JfmyAA_tvargk5lRM0-BuL66OTORGvwAgFWHQe5hVE3wPhv/s320/Deo-women.jpg" width="273" /></a></div>
<div style="color: red;">
<br /></div>
<br />
Mara nyingi wengi wetu kila baada ya kuoga na tunapokuwa na mtoko,iwe asubuhi au jioni tunapendelea kutumia deodorant katika makwapa na hata nguo kwa lengo la kuzuia harufu mbaya ya jasho. Na tumekuwa tukifanya hivyo kwa kipindi kirefu sana.<br />
JE UNAFAHAMU MADHARA YAKE?<br />
HAYA NDIO MADHARA YAKE:<br />
<br />
<span style="color: red;">MADOA KWENYE NGUO</span>: Inachukua kiasi cha sekunde 30 kwa yale majimaji ya deodorant uliyopakaa kuyeyuka katika ngozi ya mwili wako. Hivyo basi kama utapakaa deodorant katika ngozi ya mwili wako na ukavaa nguo kabla hata yale majimaji hayajakauka,inaweza kusababisha yale majimaji yakagusana na nguo na hatimaye yakatengeneza madoa sugu kwenye nguo yako. Na mara nyingi Deodorant zenye ute mweupe ndio ambazo ni hatari kwa nguo kutokana na madoa yake kuwa sugu. <br />
<br />
<span style="color: red;">MADHARA YA KIAFYA: </span>Deodorants nyingi zina 'Aluminum zirconium' ambazo zinasemekana kuwa na uwezekano wa kusababisha matatizo ya kiafya kama Anaemia,magonjwa ya mifupa na kuchanganyikiwa.<br />
<br />
<span style="color: red;">MADHARA KWENYE NGOZI</span>: Jasho kwenye mwili halina harufu ila wale bakteria ambao wanatumia jasho kama chakula ndio wanaharufu mbaya. Hivyo basi Deodorant inasaidia kufanya mwili wako kuwa acid na kupambana na bakteria. Hivyo basi Deodorant zinaweza kusababisha ngozi ya mwli wako kuwa kavu sana.<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjB-mPR3jDkLdcFK-ODhua_Bshyphenhyphenue14ILn2ukZUSyHDA0Y4OdugRd5Iue9KpF8SboJ6BX7Llhbxaf4uiYT0A7DpJm7C2nwalcMgh-eCm0DpPl_X1C4mZOEjsNY2m8thyphenhyphenlYFHlaVII1Ar9V4/s1600/deoroll.jpg" imageanchor="1" style="clear: left; float: left; margin-bottom: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="240" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjB-mPR3jDkLdcFK-ODhua_Bshyphenhyphenue14ILn2ukZUSyHDA0Y4OdugRd5Iue9KpF8SboJ6BX7Llhbxaf4uiYT0A7DpJm7C2nwalcMgh-eCm0DpPl_X1C4mZOEjsNY2m8thyphenhyphenlYFHlaVII1Ar9V4/s320/deoroll.jpg" width="320" /></a></div>
<br />
Inashauriwa kutumia Deodorant ambazo hazina viambata vya alcoholic(alcoholic free spray) ambazo baadhi ya wataalamu wanasema huwa hazina aliminium na pia zinakuwa hazina allerges au irritations.<br />
Pia inaelezwa kuwa deodorant zenye maji maji ni bora zaidi ya zile za kupuliza(spray) kwa sababu spray zina kuwa zina kemikali zenye kutoa marashi kwa muda mrefu tofauti na hizi zenye majimaji.<br />
Epuka Deodorant za bei nafuu kwa sababu itakusaidia kutotumia pesa nyingi ila inaweza kukusababishia madhara kwenye ngozi yako na afya yako kwa ujumla.<br />
<br />
<br />
<br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-62324614533075806352012-08-23T11:29:00.000+03:002012-08-23T11:29:16.387+03:00<div style="color: red;">
KUSHOTO TAZNEEM,KATIKATI OMMY DIMPOZ NA KULIA PAH ONE</div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjgtWaFcYn2dR7dZYu4va1G_b3rHRzFKgI-WDksKKx5uYfyYEUyXek_z8T2fkCeflOPtq5jj9zmskYEMhRdzTnNLL9SkZ-DFjoOmzfduQdGzMWshRQ4HjTuDXVA8SmRazTsGrSwcCRjR9ro/s1600/TAZNEEM.jpg" imageanchor="1" style="clear: left; float: left; margin-bottom: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="400" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjgtWaFcYn2dR7dZYu4va1G_b3rHRzFKgI-WDksKKx5uYfyYEUyXek_z8T2fkCeflOPtq5jj9zmskYEMhRdzTnNLL9SkZ-DFjoOmzfduQdGzMWshRQ4HjTuDXVA8SmRazTsGrSwcCRjR9ro/s400/TAZNEEM.jpg" width="340" /></a></div>
<div style="color: red;">
<br /></div>
<div style="color: red;">
<span style="color: black;">Utajiuliza kwanini nimewaweka katika pande tofauti,lakini ukweli ni kuwa ni wasanii ambao ni wapya kabisa (Up coming Artists) katika fani ya muziki wa Bongo Fleva .</span></div>
<div style="color: red;">
<span style="color: black;">Tazneem mimi ninamwona kama msanii mwenye tofauti kubwa na wasanii wengine. Kwanza pamoja na kuwa ni mtanzania ambaye ana asili ya kiasia, pia ni msanii wa kike ambaye amekuja na style ya muziki iliyo ya kipekee. Na anaonesha kuwa anao uwezo wa kuwa inspire wasanii wengine wa kike.</span> </div>
Ukitazama Video ya wimbo wake wa 'Kwasakwasa' utaweza kugundua uwezo ambao ameuonesha. Ingawa pia kwa kiwango kikubwa Producer wa wimbo amefanya kazi yake,lakini pia Tazneem ameonesha uwezo wake. Na hata kampuni iliyotengeneza video ya I-View nayo imefanya kazi yake nzuri. 'Congratulation to Audio Producers,Singer na Video Director'.<br />
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhJSu8J92ljdA_pEU8NUIkL5VEaXkHkdeh1sn1Vp4Ip_sFDo_DeN4OSmdGMsLrEVjCRhawJvmR2PTntc9B-4Ad6Eo46GEm01VibiAPucuFMBI3Ieze4ZFDkxERMfon4kJJv_jy2TeLoCHpE/s1600/DIMPOZ.jpg" imageanchor="1" style="clear: left; float: left; margin-bottom: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhJSu8J92ljdA_pEU8NUIkL5VEaXkHkdeh1sn1Vp4Ip_sFDo_DeN4OSmdGMsLrEVjCRhawJvmR2PTntc9B-4Ad6Eo46GEm01VibiAPucuFMBI3Ieze4ZFDkxERMfon4kJJv_jy2TeLoCHpE/s320/DIMPOZ.jpg" width="215" /></a></div>
Nikija upande wa Ommy Dimpoz,kwa upande wangu nadhani alipotoka na wimbo wake wa 'nai nai' wengi wetu hatukumwamini sana. Hata mimi sikuamini kama anaweza akatoa track nyingine ambayo ingeweza kuwa kali. Na kwa upande wangu ninaiona track ya pili ya 'baadae' kama ni kali zaidi ya ile ya kwanza au zipo katika kiwango kimoja, kitu ambacho wasanii wengi uwa wanashindwa. Na nimeipenda hata idea yake ya kufanyia video ya wimbo wake wa 'baadae' huko South Africa na akimtumia Director wa hapa hapa bongo Adam Juma. Hakuna ubishi kuwa kwa sasa Adam Juma ni director wa video za muziki ambaye yupo kwenye level za tofauti na directors wengine wa bongo na ukanda wote wa Afrika Mashariki.<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
</div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi1nGmaeRWJM8MnBJvMx9fb8AwEEpkurVaSXZaVRT_nq-bqWGsi8dF9SRRn47yxMp5ebTc6A2VAv4JqGqy7swFqPE3tR5f033l1K07-uE0HqkxphUWfLSV0Feyl3TkTZK2kE37yDa-RjwP9/s1600/PAHONE.jpg" imageanchor="1" style="clear: left; float: left; margin-bottom: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="213" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi1nGmaeRWJM8MnBJvMx9fb8AwEEpkurVaSXZaVRT_nq-bqWGsi8dF9SRRn47yxMp5ebTc6A2VAv4JqGqy7swFqPE3tR5f033l1K07-uE0HqkxphUWfLSV0Feyl3TkTZK2kE37yDa-RjwP9/s320/PAHONE.jpg" width="320" /></a></div>
Namalizia na Pah One ni kundi la muziki wa bongo fleva ambalo linaonekana kuwa na syle tofauti na makundi mengine ya muziki ya hapa bongo. Ukitazama namna wanavyovaa, tattoo na hata style zao za nywele. Ila nataka tusubirie track zao zitakazofuata ndio tutaweza kuwahukumu vyema zaidi. Nilichokipenda ni video ya wimbo wao wa 'ghetto'ambayo wamefanya kwa ubunifu wa kiwango cha juu. Ila tu katika upande wa audio jamaa wanaonekana kuiga syle za wasanii wa afrika kusini. Kwa ukweli sijaona jipya sana.<br />
<br />
<br />
<br />NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-54124668602848015122011-11-03T10:51:00.000+03:002011-11-03T10:51:44.344+03:00ALI KIBA UPO WAPI?<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjseweRvPI7pJerqFmG0Lkx_73LB-hMDgNgPgPqQe8eLocpnvBpPbyw0BHlO69U9HPX3tnlpXhkOoNxu7PiWR7_Ds3g2DzptD3tMZmLGz4GyF8pUjOO3ICu9sTI0GAkDURs0g7kT12g0jSt/s1600/Ali-Kiba.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjseweRvPI7pJerqFmG0Lkx_73LB-hMDgNgPgPqQe8eLocpnvBpPbyw0BHlO69U9HPX3tnlpXhkOoNxu7PiWR7_Ds3g2DzptD3tMZmLGz4GyF8pUjOO3ICu9sTI0GAkDURs0g7kT12g0jSt/s320/Ali-Kiba.jpg" width="212" /></a></div><br />
Jamaa alianza kitambo sana,tangu enzi hizo Mr Blue na Ab Skills ana shine na wakafanya wimbo wa 'Maria' Baadae jamaa akaja akatoka ki ukweli na nyimbo kali kama Cinderela,MackMuga na nyingine kali. Akafanya wimbo na Wasanii kadhaa akiwemo R-Kelly ulioitwa 'Hands across the world'. Ila mimi nilitegemea angetumia nafasi hiyo kwenda kwenye level ambayo ni ya kimataifa zaidi,ila wapi? Ali Kiba sasa hivi ana wimbo wake unaoitwa 'Dushelele' wimbo ni mzuri ila video yake kwa upande wangu sijaikubali kabisa.<br />
UNAFAHAMU SABABU ZA MIMI KUTOIKUBALI VIDEO YA WIMBO ULE?<br />
Sababu mojawapo ni rangi,kwa kweli rangi katika ile video sio nzuri katika kiwango kinachotakiwa. Hata kwa upande wa ubora,inaonekana haina ubora wa kuridhisha. Maoni yangu kwa Ali Kiba,ni kuwa anapaswa kujiboresha zaidi katika upande wa kufanya audio na video kali. Lakini pia 'promotion'inahitajika zaidi kuelekea katika level za kimataifa kwani nafasi anayo,tena kubwa zaidi. <br />
TAZAMA VIDEO YA DUSHELELE YA ALI KIBA<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/a3NQ8bin1B4?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe></div>NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-7639062145641434672011-10-26T20:51:00.000+03:002011-10-26T20:51:46.821+03:00JE UNATAMBUA KUWA SIMU YAKO YA MKONONI NI CHAFU SANA KULIKO HATA CHOO?<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgx8v8ZX3UnobxMsA4SSP1ijKQCdkc5aVlXqkBpu-CNeJ7xUf79-mZm9_VOPiTqKHogBrqF5ZZO8ClH7igQ15kx-p26Cxjm9x8w7KZwbcJbfhXyzfyxK09t_TEDh_XZGtsELHXAcwDz6t15/s1600/rear_view_of_businessman_standing_at_toilet_and_019412bl.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgx8v8ZX3UnobxMsA4SSP1ijKQCdkc5aVlXqkBpu-CNeJ7xUf79-mZm9_VOPiTqKHogBrqF5ZZO8ClH7igQ15kx-p26Cxjm9x8w7KZwbcJbfhXyzfyxK09t_TEDh_XZGtsELHXAcwDz6t15/s320/rear_view_of_businessman_standing_at_toilet_and_019412bl.jpg" width="232" /></a></div><br />
Mara nyingi sana watu wengi tuna tabia ya kusafisha mikono yetu baada ya kutoka chooni. Tunasahau kuwa wakati mwingine tunaingia huko chooni na simu zetu za mkononi,na hata kusoma sms au kutuma sms tukiwa chooni. Na tunapotoka chooni tunasafisha mikono yetu na kujiona kuwa tumeshakuwa katika hali ya usafi huku tukisahau kuwa tuliingia na simu zetu za mkononi huko chooni tulipokuwa.<br />
Utafiti mmoja umefanywa huko Uingereza,ambapo wataalamu walichukua watu 390 pamoja na simu zao za mkononi. Na hatimaye waligundua kuwa asilimia 92 ya watu waliokuwa na simu hizo waligundulika kuwa na Bakteria na asilimia 82 ya simu ziligundulika kuwa na Bakteria. Na mojawapo ya bakteria hao ni 'staphylococcus aureus' ambao wana madhara kwenye baadhi ya sehemu za mwili kama macho na kwenye ngozi.<br />
Na je unawezaje kujikinga na Bakteria hao? Imeshauriwa kusafisha mikono kila baada ya kutoka chooni. Na pia inashauriwa watu kuwa na tabia ya kusafisha simu zao angalau mara moja kwa wiki kwa kutumia kipande cha pamba kilichochovywa kwenye ''Rubbing Alcohol''NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-89871118425697326482011-10-26T12:22:00.000+03:002011-10-26T12:22:58.969+03:00SUMALEE IS NOW RIDING DIRTY WITH HAKUNAGA!!!<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwTkX682olwp7XQ2A6kM5ATopI87dlgt7rpzZmhyphenhyphen15wyKwdfcQQ-a-4QHgw6SX8UG8gtmnJbUR1xXDKO7gbaxqEdgHcjb3bpvc77YfvzKIrtNy3iwsZrYy6FDLwBDQ4ITP8hUigTeEDZgq/s1600/sumalee.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwTkX682olwp7XQ2A6kM5ATopI87dlgt7rpzZmhyphenhyphen15wyKwdfcQQ-a-4QHgw6SX8UG8gtmnJbUR1xXDKO7gbaxqEdgHcjb3bpvc77YfvzKIrtNy3iwsZrYy6FDLwBDQ4ITP8hUigTeEDZgq/s320/sumalee.jpg" width="240" /></a></div><br />
Mkali kutoka pande za Tanga ambaye maskani yake kwa sasa ni Dar-es-Salaam Ismail sadick a.k.a Sumalee ambaye kwa sasa ana datisha kila pande na songi lake la ''hakunaga''. Jamaa anastahili kupewa heshima yake,unajua kwa nini? Jibu ni kuwa ni wasanii wachache sana ambao wanaweza kupotea kwa muda mrefu kwenye gemu la mziki alafu wakawa na uwezo wa kurudi katika levo ileile iliyozoeleka.<br />
Sumalee ameanzia mbali,tangu akiwa na kundi la Parklane na enzi hizo maskani yao ikiwa mitaa ya Bombo Tanga,kundi likiwa na wasanii kibao. Na baadae akaja akaungana na Cp a.k.a Cpwaa na wakatoa albam iliyoitwa 'Nafasi nyingine'. Ikiwa na tracks kali kama Aisha Aisha,Nafasi nyingine.<br />
Tazama video ya Hakunaga!!!!<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.youtube.com/embed/-VA4JDtUjys?feature=player_embedded' frameborder='0'></iframe></div>NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-6882174038494499542011-10-26T11:44:00.000+03:002011-10-26T11:44:17.535+03:00NDEGE YA KIPEKEE;BOEING 787 DREAMLINER SASA IMEANZA SAFARI<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiocv1CPYJVV4hL5qcB6ZJZo-1J2-HmHDZ5acWpdknglcKP_EuHtu0IaQO7fYCt-zEkulLZ3mxTqR-DMjVBWWaV40cQ427aH9ftXQ-fBlhaLGDASXo6Qj0gkJ0fxeSc-dpA918_wozyLeZZ/s1600/boeing_787.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="252" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiocv1CPYJVV4hL5qcB6ZJZo-1J2-HmHDZ5acWpdknglcKP_EuHtu0IaQO7fYCt-zEkulLZ3mxTqR-DMjVBWWaV40cQ427aH9ftXQ-fBlhaLGDASXo6Qj0gkJ0fxeSc-dpA918_wozyLeZZ/s320/boeing_787.jpg" width="320" /></a></div><br />
BOEING 787 DREAMLINER ambayo imekuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu na wadau wa Teknolojia duniani sasa imezinduliwa rasmi mjini Tokyo nchini Japani. Na imeanza safari zake kwa huko huko Japan katika miji ya Okayama na Hiroshima. Ndege hiyo iliyotengenezwa kipekee na material ya carbon fiber-reinforced plastic ikiwa inatumia mafuta kidogo kulinganisha na ndege nyingine za Boeing kwa takribani pungufu ya 20%. Hata madirisha yake ni makubwa kuliko ya Boeing 767 na yanapitisha mwanga wa kutosha na nindege yenye kuingiza hewa ya kutosha kulinganisha na ndege nyingine. Na pia ina uwezo wa kusafiri kilomita 15000 bila kutua mahali popote. Ndege hiyo inamilikiwa na shirika la ndege liitwalo ANA ambalo limeagiza ndege nyingine kama hizo 55. <br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg34ygylESplCOpdOFRRMxauJpaAk22OIMqa34J-nI0Fene-ql3oneCLXr5ctJWm2d4uYHmJxsCU6SZHnJQ80mkV8gIC5KUAtRD2Wrzhf-2wCTgAbCJwkN2c_FcxM2VT-PXEvmhPaE5gu0J/s1600/Boeing-787-Capacity.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="240" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg34ygylESplCOpdOFRRMxauJpaAk22OIMqa34J-nI0Fene-ql3oneCLXr5ctJWm2d4uYHmJxsCU6SZHnJQ80mkV8gIC5KUAtRD2Wrzhf-2wCTgAbCJwkN2c_FcxM2VT-PXEvmhPaE5gu0J/s320/Boeing-787-Capacity.jpg" width="320" /></a></div><div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiVx9aLnBL0Ux_ZJGuPYdZIBb02NHCrpRtMDdpFTSWIDmaL1IGhZq3EdqC-zxqMh2l_IoJqGqXV9kBTFbjEf3WIR-L1yPrbJNw21Uen1tZksd-0yQDtq2kH4qzT9cbIJCrrYCHKBvv9u42Y/s1600/dreamliner-cockpit-2.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="240" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiVx9aLnBL0Ux_ZJGuPYdZIBb02NHCrpRtMDdpFTSWIDmaL1IGhZq3EdqC-zxqMh2l_IoJqGqXV9kBTFbjEf3WIR-L1yPrbJNw21Uen1tZksd-0yQDtq2kH4qzT9cbIJCrrYCHKBvv9u42Y/s320/dreamliner-cockpit-2.jpg" width="320" /></a></div>NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-78086936880289049452011-10-24T23:49:00.000+03:002011-10-24T23:49:56.826+03:00UNAMKUMBUKA MC HAMMER? SASA YUPO KWENYE LIGI NA WAMILIKI WA GOOGLE<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUJnQzhHqGCA6SP67RZXCkt4WYekSNE-aZ90Uh3-i2dGGxShIUN_bLw3JU-ZBA4m8G6K6JvBVUpQi2Y7KBgTkYK0zvq5PVstiG4nx2eywgKb_YOSovZ8u06mNSx2uC1g-u0RR-tc62DQ6M/s1600/MC-Hammer-a06.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUJnQzhHqGCA6SP67RZXCkt4WYekSNE-aZ90Uh3-i2dGGxShIUN_bLw3JU-ZBA4m8G6K6JvBVUpQi2Y7KBgTkYK0zvq5PVstiG4nx2eywgKb_YOSovZ8u06mNSx2uC1g-u0RR-tc62DQ6M/s320/MC-Hammer-a06.jpg" width="240" /></a></div><br />
Mc Hammer sasa ameingia kwenye mambo ya teknolojia baada ya kutangaza kuanzisha search engine iitwayo 'WireDoo'. Mc Hammer alitangaza kuanzishwa kwa search engine hiyo katika mkutano mkubwa unaoitwa WEB 2.0 huko San Fransisco Marekani. Kwa mujibu wa Mc Hammer amesema WireDoo itakuwa inatumika kutafuta topiki au vitu mbalimbali mfano magari na vitu vingine tofauti.<br />
Mc Hammer ambaye alikuwa ni mkali wa Hiphop aliyefunika mbaya miaka hiyo? kwa sasa anajishughulisha na mambo ya teknolojia. Na ameshaudhuri kwenye vyuo mbalimbali kutoa mihadhara (presentations) ikiwemo Oxford University cha England na Harvard cha Marekani.<br />
Kwa sasa hivi Google ndio kila kitu,pale unapozungumzia social engine kali. Je WireDoo inaweza ikaipiga bao Google????NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-20996939505645698052011-10-24T23:15:00.000+03:002011-10-24T23:15:58.114+03:00UTAFITI :TOVUTI ZA PORNO ZINA ATHARI KWA VIJANA<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiTFhcnkzIJ-kwZx-dtcvA40DtTvR8jR0pPBsdFzv0_f6cAT6oTeBScsRAjx4RuwOmaw6r163xv2EFVzJiG1Ys8-vIur_37nB0MpkgWGTzjuDJyqox0yvzq-SDCVyihDcMKcXVSBiWDISAH/s1600/boy-asleep-at-computer.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="259" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiTFhcnkzIJ-kwZx-dtcvA40DtTvR8jR0pPBsdFzv0_f6cAT6oTeBScsRAjx4RuwOmaw6r163xv2EFVzJiG1Ys8-vIur_37nB0MpkgWGTzjuDJyqox0yvzq-SDCVyihDcMKcXVSBiWDISAH/s320/boy-asleep-at-computer.jpg" width="320" /></a></div><br />
Utafiti uliofanywa na Chuo kikuu cha Padua kilichopo nchini Italia umeonesha kuwa vijana wengi wana athirika sana kisaikolojia kutokana na kutazama na kufuatilia kupita kiasi tovuti za porno. Utafiti huo uliofanywa nchini Italia na kwingineko unaonesha kuwa vijana wengi wanapokuwa katika umri wa miaka 11-19 wanakuwa wanatazama picha za porno ambazo uwaletea madhara baadae. Kiasi cha kuathirika kisaikolojia na hata kushindwa kupafomu tendo lenyewe kihalisia. Utafiti unaonyesha wanaume wengi huko Italia ambao walikenda kwa wataalamu wa mambo ya saikolojia kwa ajili ya kutafuta ushauri iligundulika kuwa wengi wao wameathirika na kutazama kufuatilia tovuti za porno.<br />
Tovuti za porno zimeshauriwa kutoruhusu wanaume chini ya miaka 35 kutembelea tovuti hizo kwa sababu za kiafya.<br />
VIPI KWA HAPA TANZANIA??????????????????NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3730042189525741866.post-36952347284285603332011-10-18T11:35:00.000+03:002011-10-18T11:35:56.781+03:00BLACKBERRY INAZIDI KUPOTEZA MVUTO AU TATIZO NINI?<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjC5SpfP1nMD9VkuR3VoNsrzWmFdt77Pa3OwbY9roOv4mXmTsF5_M0YlsFiVMLcvwmNBSSX_M2Kgy88hVt2aZ8pumDyr_J2KQAMtHgYewSirF-d5dRJeMfU6_72S3Arg5NRqTtkyM0dS9s-/s1600/blackberry-bold-9700.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="280" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjC5SpfP1nMD9VkuR3VoNsrzWmFdt77Pa3OwbY9roOv4mXmTsF5_M0YlsFiVMLcvwmNBSSX_M2Kgy88hVt2aZ8pumDyr_J2KQAMtHgYewSirF-d5dRJeMfU6_72S3Arg5NRqTtkyM0dS9s-/s320/blackberry-bold-9700.jpg" width="320" /></a></div><br />
Mmoja kati ya watumiaji watano wa BlackBerry ambaye alipata matatizo ya mawasiliano wiki nzima iliyopita amedai kuna akaacha kutumia aina hiyo ya simu. Hii ni baada ya mamilioni ya watumiaji wa BlackBerry kukosa mawasiliano ya internet kwa takribani wiki nzima iliyopita. Kwa mujibu wa survey iliyofanywa kwa zaidi ya watu 1000 na mtandao wa kelkoo imeonekana kuwa 8% tayari wameshaacha kutumia BlackBerry,huku 19% wakidai wanafikiria kuachana na matumizi ya BlackBerry na 42% wakidai uenda wakaachana na BlackBerry hapo baadae iwapo itaendelea kuwa na matatizo . Katika nchi za ulaya na Marekani baada ya uzinduzi wa Iphone 4S ambayo ni aina mpya ya simu kutoka Apple tayari idadi ya wanaohitaji aina hiyo ya simu imeongezeka sana na kufikia milioni moja hususani baada ya watumiaji wa BlackBerry kukumbwa na matatizo ya mawasiliano wiki iliyopita. Hivi karibuni kampuni ya RIM ambayo inatengeneza BlackBerry imeomba radhi kwa watumiaji wake na kuahidi kutoa software mpya bure kwa watumiaji wake kama ishara ya kuonyesha kuwajali. Lakini kwa mujibu wa wataalamu wa mambo ya mawasiliano wamedai hilo haliwezi kuwasaidia BlackBerry katika kukuza mauzo yake,kwani watumiaji wengi wa BlackBerry ni wafanyabiashara ambao mawasiliano kwa njia ya internet ni muhimu kwao.<br />
Hata hivi karibuni thamani ya hisa za BlackBerry inaonekana kushuka kwa kasi.NOEL NEKhttp://www.blogger.com/profile/10432939962645805402noreply@blogger.com0